Thursday, July 18, 2013

Mashahidi 2 wajiondoka kwa kesi ya Kenyatta


Fatou Bensouda
Kiongozi wa mashtaka katika mahakama ya kimataifa ya ICC Fatou Bensouda, amesema kuwa mashahidi wawili wametupilia mbali ushahidi wao katika kesi dhidi ya rais wa Kenya Uhuru Kenyatta
Bi Bensouda alisema mashahidi nambari 5 na 426 wamefutilia mbali ushahidi wao kwa sababu za waswasi kuhusu usalama wao.
"kwa kifupi, inaonekana kuwa wasiwasi wa shahidi nambari tano, wameogopa sana kuhusu usalama wao na kuwa athari za kutoa ushahidi wake huenda zikawa na madhara makubwa kwa maisha yake na kwa hivyo akaamua kufutia mbali ushahidi wake.'' alisema Bensouda kwa ujumbe wake kwa majaji mnamo Jumanne.
Aliongeza kuwa upande wa mashtaka, ulikuwa umefanya mashauriano na shahidi nambari 426 kumtaka abadili msimamo wake, lakini mazungmzo hayakufua dafu.
"upande wa mashtaka umefanya mazungumzo na shahidi 426 kujua ikiwa hatua zozote zinaweza kuchukuliwa kuodnoa wasiwasi wake pamoja na kumwezesha kuhudhuria kesi. Mazungumzo hayo, hata hivyo hayakufua dafu baada ya kusisitiza kuwa hayuko tayari kutoa ushahidi wake, '' aliongeza kusema Bi Bensouda said.
Hata hivyo mwendesha mashtaka aliwaaambia majaji kuwa ushahidi wao sio muhimu tena kwa ushahidi wake dhidi ya mtuhumiwa.
Kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta itaanza kusikilizwa Novemba 12.

Friday, July 12, 2013

Malema azindua chama cha kisiasa


Julius Malema kiongozi wa chama cha EFF
Aliyekuwa kiongozi wa vugu vugu la vijana la chama tawala nchini Afrika Kusini cha ANC, Julius Malema amezindua kundi la kisiasa litakalojulikana kama Wapiganiaji wa Uhuru wa Kiuchumi au Economic Freedom Fighters, EFF.
Malema, ambaye alitimuliwa kutoka kwa chama cha ANC, mwaka wa 2012, amesema chama chake cha EFF kinataka zoezi la kugawanya mashamba kuanzisha upya na pia kutaifishwa kwa migodi yote ya madini.
''Tutagawana ardhi sisi zote ukiwa mweusi au mweupe. Lakini ukikataa kugawanya itamaanisha kuwa utalazimishwa kufanya hivyo'' Alisema Bwana Malema.
Ametaja dhamira kuu ya vugu vugu hilo kuwa kupamabana mfumo wa kipebari.
Akiwa amevalia kofia nyekundu iliyo na maandishi ''Amirijeshi Mkuu wa EFF'' Bwana Malema amewaambia waandishi wa habari kuwa chama chake kimebuniwa ili kutetea maslahi ya raia wanaoteseka katika maeneo ya mashinani.

EFF kukupambana na ANC katika uchaguzi mkuu

Rais wa Afrika Kusini na Kiongozi wa chama cha ANC Jacob Zuma
Malema ambaye alikuwa mmoja wa washirika wa karibu wa rais Zuma, kwa sasa ni mmoja wa wakosoaji wakubwa na aliongoza mikakati ya kumuondoa kama kiongozi wa chama cha ANC wakati wa mkutano wa baraza kuu la chama hicho mwaka wa 2012.
Malema ameshutumu rais Zuma kwa kutoimarisha juhudi za kuwasaidia raia weusi wa nchi hiyo ambao ni masikini na waliompigia kura.
Hata hivyo haijabainika ikiwa atawania kiti chochote katika uchaguzi mkuu utakaoandaliwa mwaka ujao, akisema kuwa uamuzi huo utatolewa baada ya mkutano wa baraza kuu la chama hicho cha EFF utakaofanyika mwisho wa mwezi huu.
Wachanganuzi wa kisiasa wanasema idadi kubwa ya raia wa Afrika Kusini, wamepoteza imani na chama cha ANC, ambacho kimekuwa madarakani tangu mwaka wa 1994.
Rais wanasema maafisa wengi wa chama hicho ni wafisadi na hawana nia ya kuimarisha hali ya maisha.

Serikali yarejesha mawasiliano ya Simu


Ramani ya Nigeria
Serikali ya Nigeria imesitisha mpango wake wa kuzuia mawasiliano ya simu katika jimbo moja kati ya majimbo matatu ambayo hali ya hatari imetangazwa kwa sababu ya mashambulio ya mara kwa mara kutoka kwa wanamgambo.
Jimbo la Adamawa halijaadhiriwa pakubwa na mashambulio hayo yanayofanywa na wapiganaji wa Kiislamu wa Boko Haram.
Wiki iliyopita, afisa mmoja mwandamizi wa serikali alisema kuwa ukosefu wa mawasiliano ya simu, ulizuia raia kutoa habari kwa serikali wakati shule moja ilipovamiwa.
Lakini jeshi la nchi hiyo limesema, uamuzi huo ulichukuliwa ili kuzuia wanamgambo hao kupanga mashabulio hayo.
Kundi la Boko Haram linadaiwa kuwaua zaidi ya watu elfu mbili tangu ilipoanzisha mashambulio yake mwaka wa 2009.
Wizara ya Ulinzi nchini Nigeria, limesema hali ya ulinzi imeimarika katika jimbo hilo la Adamawa.
Mwandishio wa BBC nchini Nigeria, alifanikiwa kuwasiliana na mkaazi mmoja wa jimbo hilo la Adamawa mapema siku ya Ijumaa.
Hata hivyo mawasiliano katika majimbo jirani ya Yobe na Borno bado yamekatizwa.
Mwezi Juni mwaka huu jeshi la nchi hiyo lilitangaza kuwa mtu yeyote atakayepatikana na simu ya Satellite katika jimbo la Borno atakamatwa.
Baadhi ya simu zilizopigwa marufuku Nigeria
Wiki iliyopita, Gavana wa Jimbo la Yobe Ibrahim Gaidam aliagiza shule zote za sekondari kufungwa baada ya wanafunzi ishirini na wawili kuuawa na shule yao kuteketezwa na wapiganaji wa Boko Haram.
Gavana huyo hata hivyo alitoa wito kwa serikali kurejesha mawasiliano ya simu ili kusaidia raia kutoa habari kwa utawala wakati kunapotokea mashambulio.
Mawasiliano ya simu za nyaya nchini Nigeria mara nyingi hazifanyi kazi nje ya miji mikuu ya Abuja na Lagos.
Wanajeshi zaidi wametumwa katika majimbo ya Kaskazini mwa Nigeria tangu serikali ilipotangaza hali ya tahadhari.
Kundi la Boko Haram, ambalo majina yake yanamaanisha Elimu ya mataifa ya Magharibi hairuhusiwa, inataka sheria za Kiislamu kutumika katika eneo la Kaskazini lenye idadi kubwa ya waumini wa dini ya Kiislamu.

Mwana Mfalme akamatwa California


Meshael Alayban
Mama mmoja ambaye ametajwa kuwa mwana mfalme kutoka Saudi Arabia amekamatwa katika jimbo la California nchini Marekani na kutuhumiwa kuhusika na ulanaguzi wa watu.
Meshael Alayban, 42, anakabiliwa na mashtaka ya kumlazimisha mama mmoja kutoka Kenya kufanya kazi kwa zaidi ya masaa kumi na sita kila siku, na kumlipa kiasi kidogo cha pesa kuliko walivyokuwa wameafikiana.
Utawala wa eneo hilo, umesema kuwa Bi Alayban alichukua pasi ya kusafiria ya mama huyo, hatua iliyomfanya atoroke.
Mawakili wa mwana mfalme huyo wametaja kesi hiyo kuwa mzozo kuhusu hali ya utendaaji kazi.
Novemba mwaka uliopita, wapiga kura katika jimbo la California, waliidhinisha sheria kali dhidi ya watu watakaopatikana na hatia ya kuhusika na ulanguzi wa watu.
Ikiwa atapatikana na hatia, Bi Alayban, huenda akahukumiwa kifungo cha miaka kumi na miwili gerezani, adhabau ambayo ni asilimia mia moja zaidi kuliko ilivyokuwa kabla ya wapiga kura kuidhinisha mageuzi sheria hiyo mpya.
Waendesha mashtaka wanasema Bi Alayban, ni mmoja wa wake sita wa Mwana Mfalme Abdulrahman bin Nasser bin Abdulaziz al-Saud, mmoja wa wanawe wa kiume wa familia moja ya kifalme nchini Saudi Arabia.

Mtumwa

Mama huyo kutoka Kenya ambaye jina lake halijatolewa, aliajiriwa na Bi Alayban miaka miwili iliyopita, baada ya kusaini mkataba na shirika moja la kutoa uajiri nchini Saudia.
Mama huyo alihaidiwa kulipwa dola elfu moja mia sita kila mwezi na kuwa atafanya kazi masaa manane kila siku kwa siku tano.
Lakini, Bi Alayban amekuwa akimlipa dola mia mbili ishirini kila mwezi na kulazimishwa kufanya kazi kwa zaidi ya masaa kumi na sita kila siku.
Mama huyo kutoka Kenya vile vile amedai, kupokonywa pasi yake ya kusafiria na alikabithiw muda mfupi tu kabla ya wao kusafiri kwenda Carlifonia na Bi Alayban.
Akiwa California, alilazimishwa kufanya majukumu mengi zaidi ya kinyumbani kwa familia ya watu wanane waliokuwa katika vyumba vinne tofauti, ambako amedai alizuiliwa mateka.
Wakati alifanikiwa kutoroka, alisimamisha basi moja na kwenda moja kwa moja hadi kituo cha polisi.
Biu Alayban alikamatwa siku ya Jumatano na kufikishwa mahakamani siku ya Alhamisi.
Aliachiliwa huru kwa dhamani ya dola milioni tano na kuamriwa kurejesha pasi ya kusafiria ya amama huyo kutoka Kenya.
Aidha Bi Alayban sasa atavalia chombo maalum ambacho kitatoa maelezo ya mahala aliko na hataruhusiwa kuondoka Marekani hadi kesi hiyo itakapokamilika.
Viongozi wa Mashtaka walitaka jaji kumuachilia kwa dhamani ya dola milioni Ishirini au anyimwe dhamana kwa kuwa yeye ni tajiri mkubwa na aweza kutoweka.

Friday, June 7, 2013

Maandamano sharti yakome'', Erdogan


Maandamano yamekumba mji wa Istanbul kwa zaidi ya waiki moja sasa
Waziri Mkuu wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan ametaka maandamano yanayoendelea nchini humo kumalizika mara moja.
Akiwahutubia maelfu ya wafuasi wake waliomlaki katika uwanja wa ndege wa Istanbul,kiongozi huyo amesema maandamano hayo sio halali.
Lakini alipokuwa akiongeza maelfu ya waandamanaji wanaopinga serikali walikuwa wanakusanyika mjini Istanbul katika bustani ya Taksim.
Maandamano hayo yalianza kama maandamano madogo kuhusu bustani moja mjini Istanbul ingawa yakaongezeka na kuwa maandamano makubwa.
Wafuasi 10,000 wa chama cha Bwana Erdogan, walikwenda uwanjani kumkaribisha baada ya ziara yake ya Kaskazini mwa Afrika.
Akisimama kando ya mkewe na mawaziri wa serikali, aliwaambia wafuasi wake kuwa maandamano hayo ni kinyume na sheria na lazima yakomeshwe mara moja.
"sisi hatujawahi kuunga mkono mgawanyiko katika jamii lakini hatuwezi kuunga mkono watu wenye nia ya kuwagawanya watu.''
Erdogan aliwasihi wafuasi wake kuwa watulivu baada ya kuelezea nia yao ya kutaka kulipiza kisasi.
"mmekuwa watulivu , mmeonyesha ukomavu na kutumia akili zenu, sote tutakwenda nyumabi kutoka hapa.''
Bwana Erdogan alijibu wito wa watu kutaka ajiuzulu akiwakumbusha uchaguzi wa mwaka 2011 ambapo alishinda uchaguzi huo kwa asilimia hamsini.
''Wanasema kuwa mimi ni waziri mkuu wa asilimia hamsini ya nchi. Tumewahudumia watu milioni 76 kutoka Mashariki hadi Magharibi,'' alisema Erdowan
Ilikuwa mara ya kwanza wafuasi wa Erdogan wamemuunga mkono, kufuatia wiki moja ya maandamano ambayo yamemtaka aondoke mamlakani.
Mwandishi wa BBC Mark Lowen mjini Istanbul, anasema kuwa kukaribishwa kwa waziri mkuu,kwa namna hiyo ni ishara ya uungwaji mkono alionao kutoka kwa wafuasi wake.
Hata hivyo,baadhi wanasema kuwa matamshi ya Bwana Erdogan huenda yakachochea maandamano hayo zaidi.
Migawanyiko nchini Uturuki, inaonekana kukithiri zaidi katika siku zijazo na huenda hali ikawa ya hatari kubwa.

US harvesting data from Facebook, Google and other internet giants


America's secret surveillance state was dragged further out of the shadows on Thursday as it emerged that the US is reaching directly into the servers of Facebook, Google and other internet companies to harvest data.
Facebook Mark Zuckerberg
Facebook is among at least nine tech companies that make up the NSA's PRISM programme. 
The National Security Agency's (NSA) classified PRISM programme reportedly allows the government to collect virtually limitless amounts of information from emails, pictures and social media accounts.
The disclosure of the programme comes one day after it emerged that the government has been tracking the phone calls of millions of Americans for the last seven years, sparking accusations the Obama administration is trampling civil liberties.
Unlike the phone tracking programme, where telecom companies are forced to hand over records, PRISM appears to allow the NSA to freely search the tech firms' networks at any time.
PRISM also allows the government access to the content of online accounts, whereas the phone programme provides data on the time and location of a call but does not tell investigators what was said.
A secret slide show obtained by The Guardian and The Washington Post appear to indicate that the nine companies are willing participants in the programme, beginning with Microsoft in 2007.

Tuesday, June 4, 2013

Evidence that chemical weapons have been used in Syria attacks reaches UN

Chemical weapons have been used in at least four attacks Syria as crimes against humanity are perpetrated every day, according to a UN inquiry.
Free Syrian Army fighters preparing  to fire on Syrian army positions in the old city area of Aleppo
Free Syrian Army fighters preparing to fire on Syrian army positions in the old city area of Aleppo Photo: EPA
The UN Commission of Inquiry on Syria said in a report that both sides were deliberating breaking the rules of war against millions of victims.
"War crimes and crimes against humanity have become a daily reality in Syria," the Commission of Inquiry on Syria said in a report delivered to the UN Human Rights Council in Geneva, adding it had "reasonable grounds to believe that chemical agents have been used as weapons.
The regime of President Bashar al-Assad was accused of a "concerted policy" of massacre and forced displacement of civilians against the nationwide rebellion it faced. Meanwhile rebels could also have used chemical weapons as well as the regime.
In their latest report, based on interviews with victims, medical staff and other witnesses, they said they had received allegations that Syrian government forces and rebels had used the banned weapons, but that most testimony related to their use by state forces.
"There are reasonable grounds to believe that limited quantities of toxic chemicals were used. It has not been possible, on the evidence available, to determine the precise chemical agents used, their delivery systems or the perpetrator," Paulo Pinheiro, who chairs the U.N. commission of inquiry, told a news conference in Geneva.