20 Aprili, 2013 - Saa 15:37 GMT
Shirika la habari la taifa la Uchina linasema kuwa watu 150 wamekufa katika tetemeko kubwa la ardhi ambalo limeporomosha majengo na bara-bara katika jimbo la Sichuan, kusini-magharibi mwa nchi.
Shughuli za uokozi zinatatanishwa na bara-bara zilizovunjika na simu zilizokatika.
Waziri Mkuu, Li Keqiang, aliwasili huko haraka kuongoza shughuli hizo.
Tetemeko lilotokea katika jimbo la Sichuan mwaka wa 2008 liliuwa watu 90,000
No comments:
Post a Comment