Saturday, April 20, 2013

Tetemeko kubwa laitikisa Uchina

 20 Aprili, 2013 - Saa 15:37 GMT


Shirika la habari la taifa la Uchina linasema kuwa watu 150 wamekufa katika tetemeko kubwa la ardhi ambalo limeporomosha majengo na bara-bara katika jimbo la Sichuan, kusini-magharibi mwa nchi.
Shughuli za uokozi baada ya tetemeko
Wanajeshi kama 6000 wamepelekwa kwenda kusaidia katika uokozi zaidi ya kilomita 100 kutoka Chengdu, mji mkuu wa jimbo la Sichuan.
Shughuli za uokozi zinatatanishwa na bara-bara zilizovunjika na simu zilizokatika.
Waziri Mkuu, Li Keqiang, aliwasili huko haraka kuongoza shughuli hizo.
Tetemeko lilotokea katika jimbo la Sichuan mwaka wa 2008 liliuwa watu 90,000

No comments:

Post a Comment