Friday, April 19, 2013

Rais wa Somalia azindua mpango wa kupunguza matumizi ya mkaa

Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud alizindua siku ya Jumatano (tarehe 17 Aprili) mpango wa matumizi ya mkaa unaosaidiwa na mashirika matatu ya Umoja wa Mataifa.
    Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud (kulia) akipanda mti katika ikulu ya rais ya Villa Somalia mjini Mogadishu hapo tarehe 17 Aprili kwa kumbukumbu ya Siku ya Miti. [Na Ofisi ya Rais wa Somalia/Jalada]
  • Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud (kulia) akipanda mti katika ikulu ya rais ya Villa Somalia mjini Mogadishu hapo tarehe 17 Aprili kwa kumbukumbu ya Siku ya Miti. [Na Ofisi ya Rais wa Somalia/Jalada]
Robo milioni ya tani za mkaa husafirishwa kwenda nchi za Ghuba kila mwaka, kwa mujibu wa ofisi ya UN Somalia. Ili kuzalisha kiasi hicho, idadi ya miti milioni 4.4 hukatwa katika ardhi iliyosafishwa ya hekta 72,900, na kuzidisha uwezekano wa uharibifu kutokana na ukame na mafuriko.
Mohamud aliahidi wajibu wa serikali yake ya kusimamisha kabisa usafirishaji nje wa mkaa.
"Kuna sheria katika nchi hii ambazo zilipitishwa miaka ya 1970 na serikali ya Somalia. Pia kumekuwepo na maazimio ya UN kuhusu upigwaji marufuku mkaa," Mohamud alisema katika taarifa fupi ya kuadhimisha Siku ya Miti. "Licha ya hali ya sasa, lazima tuziimarishe sheria hizi."
Shirika la Chakula na Kilimo, Mpango wa UN wa Mazingira na Mpango wa Maendeleo wa UN yanasaidia juhudi za serikali ya Somalia za kuwezesha ushirikiano wa kikanda, kutengeneza vyombo vya udhibiti na taratibu za utekelezaji, kuanzisha vyanzo mbadala vya nishati na kuwasaidia wafaidikaji wa biashara ya mkaa kutafuta njia mbadala za kujipatia riziki.
Uzalishaji mkaa unaharakisha mchakato wa kuenea kwa jangwa, kupungua kwa ardhi ya kilimo au malisho ya wanyama na kuwasukuma wakaazi kutoka maeneo yao kwa vile haikaliki. Al-Shabaab pia wamekuwa wakitegemea usafirishaji haramu wa mkaa ili kugharamia shughuli zao za kigaidi.
"Nataka niseme hivi, usafirishaji mkee nje ni kosa la jinai, " Mohamud alisema. "Ardhi yetu na urithi wa kilimo vinategemea miti yetu. Lazima tuyalinde mazingira yetu kuimarisha sheria za ndani za kimataifa."
Rais wa Somalia alipanda mti katika ikulu ya rais ya Villa Somalia na kuwahamasisha wananchi kupanda miti katika vitalu vyao na ardhi yao pia.

No comments:

Post a Comment