Thursday, April 4, 2013

Ziara ya Rais wa China nchini Tanzania imeleta mafanikio mengi kwa Zanzibar

 
 
 
 
 
 
Rate This

china
Imeelezwa kuwa ziara ya Rais wa China nchini Tanzania imeleta mafanikio mengi kwa Zanzibar ikiwa ni pamoja na Makampuni ya Kichina kupanga kuwekeza katika sekta tofauti Zanzibar.

Balozi Mdogo wa China anayefanya kazi Zanzibar Bi Chen Qiman ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisini kwake Mazizini kuhusiana na matokeo ya ziara ya Rais Jinping aliyofanya karibuni nchini Tanzania.
Amesema Zanzibar imeweza kunufaika moja kwa moja na zira hiyo ikiwa ni pamoja na kusainiwa Miradi mitatu ya maendeleo kwa ajili ya Visiwa vya Unguja na Pemba.
Bi Chen amesema Rais wa China pia amemualika Rais Shein kwenda China kwa ziara ya kikazi ambapo pia atapata fursa zaidi ya kupanga mambo mengi ya kimaendeleo nchini huko.
Ameongeza kuwa Ziara hiyo inayotarajiwa kufanyika mwaka huu itakuwa fursa adhimu kwa Rais Shein kujifunza mengi na kukuza mahusiano zaidi kati ya Zanzibar na Jamhuri ya China.
Akizungumzia mikakati iliyowekwa na China ya kuisadia Zanzibar Bi Chen amesema Ofisi yake itaendelea kuitangaza Zanzibar katika nchi yake ili kuwavutia Wananchi wa China kuja kutembelea Zanzibar na kuimarisha Sekta ya Utalii.
katika kufanikisha hilo Bi Chen ameshauri Wazanzibari kuijifunza Lugha ya Kichina ili kurahisisha mawasiliano iwapo Wageni hao watakuja kutalii nchini hapa.
Mikakati mingine waliyoipanga ni pamoja na kuyahamasisha Makampuni kufanya uwekezaji katika Viwanda vya kusindika Matunda na kuwekeza katika Bahari jambo ambalo litasaidia sana maendeleo na kupunguza ukosefu wa Ajira.
Ziara ya Rais Jinping nchini Tanzania aliyoifanya karibuni imezidi kuimarisha mahusiano mema kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya China ambapo katika ziara hiyo jumla ya Miradi 17 ya kimaendeleo iltiwa saini.

No comments:

Post a Comment