Tuesday, November 13, 2012

SIRA FUPI YA MTUME MUHAMMAD (SAW)

SIRA YA MTUME (SAW)

Sira ni fani inayojishughulisha kuelezea maisha ya Nabii Muhammad tangu kuzaliwa mpaka kufa kwake, ikiwa ni pamoja na malezi na makuzi yake, wasifu wake wa kimaumbile, tabia zake, harakati zake katika kuufikisha ujumbe wa Uislamu kwa ummah, mahusiano yake na watu na mataifa mbalimbali. Pia sira inaelezea hali ya ulimwengu kijamii na kiitikadi kabla na baada ya kuja Nabii Muhammad, kadhalika inataja maisha na utawala wa Makhalifa waongofu baada ya Mtume.

Fani ya Sira inalenga kumfahamisha Muislamu:-
  1. Taswira na mfumo mzima wa Uislamu unatolewa na kutafsiriwa na maisha ya Mtume.
  2. Maisha ya Nabii Muhammad ndio kigezo na mfano mwema wa kuigwa na kufuatwa ili kuweza kupata mafanikio Duniani na Akhera. Mwenyezi Mungu atuambia:-"BILA SHAKA MNAO MFANO MWEMA KWA MTUME WA MWENYEZI MUNGU…"(33:21)
  3. Muislamu apate katika maisha ya Nabii Muhammad kitu kitakachomsaidia kuifahamu Qur-ani kwani aya nyingi za Qur-ani zinafasiriwa na kuwekwa wazi na matukio yaliyotokea katika uhai wa Mtume.
  4. Sira inaonyesha ni njia na mbinu zipi alizozitumia Mtume mpaka akaweza kuusimamisha Uislamu katika ulimwengu uliokuwa umefunikwa na kiza totoro cha ushirikina.
  5. Sira inaonyesha ni jinsi gani Mtume alivyoyatatua matatizo na vikwazo mbalimbali vya ndani na nje alivyokumbana navyo katika kumfikisha ujumbe wa Allah kwa watu wote.
Hizi ni baadhi tu ya faida zinazopatikana katika kuisoma na kuifuata sira ya Bwana Mtume.


i  )BARA ARABU WAKATI WA MTUME NA WAKAZI WAKE

Bara Arabu lipo upande wa kusini wa Bara la Asia. Bara hili ndilo makazi ya Waarabu tangu kale na mpaka sasa kinaishi humo kizazi cha Waarabu. Maelfu ya miaka Waarabu wa kale wliishi maisha yaliyofanana na maisha yetu ya leo ukiondoa tofauti chache zilizokuwepo. Walikuwepo miongoni mwao wakazi wa mijini waliostaarabika na kuendelea.
Ama zile tofauti chache zilizokuwepo kati ya maisha ya Waarabu wale wa kale na maisha yetu ya leo ni kwa upande wa kidini (kiitikadi) na kijamii. Waarabu wa kale waliishi katika enzi/zama za viza zilizotawaliwa na itikadi potofu za kidini na desturi mbaya. Baada ya kudhihiri Uislamu hali mbaya hizi zilibadilika na Waarabu wakaanza kuishi katika zama za uchanuzi wa dini ya Kiislamu katika mji wa Makkah kisha ikaenea katika pande zote za Bara Arabu Uislamu ulizibadilisha hali na kupigiwa mfano.

Mji wa Makkah ndio kitovu na chimbuko la kuenea dini ya Kiislamu. Mji huu upo katika nchi ya Hijazi, nchi ambayo imechukua eneo kubwa la Bara Arabu. Nchi hii ya Hijazi ilikaliwa na makabila mengi ya Kiarabu, kabila mashuhuri zaidi lilikuwa ni Qurayshi.
Historia ya mji wa Makkah na kuanzishwa kwake inaanzia pale alipofika katika mji huo kwa mara ya kwanza Nabii Ibrahimu – Amani na Rehma za Allah zimshukie -   akitokea nchi ya Palestina akiwa pamoja na mkewe Haajira na mwanawe Ismail. Wakati huo mji wa Makkah ulikuwa ni jangwa tupu lililozungukwa na majabali. Nabii Ibrahimu akamuacha mkewe na mwanawe katika jangwa hilo tupu lisilo na mimea na kurejea Palestina. Kabla ya kufunga safari ya kurudi Palestina Nabii Ibrahimu alimuomba Mola wake Mtukufu rehema zake ziyatawale maisha mapya ya mkewe na mwanawe jangwani hapo na Mola Muumba aliipokea na kuikubali dua ya Mtume wake kama tunavyosoma ndani ya Qur-ani. Mwenyezi Mungu akamchimbulia mama Haajira na mwanawe Ismail chemchem ya Zamzam katika ardhi kame ya jangwani.
Wasafiri wapitao njia ile walipokiona kisima cha Zamzam walikwenda mahala pale na kuamua kuishi kandokando ya chemchem ile, hii ni kutokana na shida sugu ya maji jangwani. Tangu wakati huo kitongoji hicho kikaanza kustawi mpaka kikawa ndio kitongoji mama cha nchi ya Hijazi. Mtoto Ismail alipofikia umri wa kuoa alioa katika makabila yale ya Waarabu waliokuja kukaa pale na kuuanzisha mji wa Makkah. Akajaaliwa kupata watoto.
Ibrahimu baba yake Ismail akawa anafanya ziara za mara kwa mara kujulia hali mkewe, mwanae na wajukuu zake. Katika mojawapo ya ziara zake hizi ndipo Mwenyezi Mungu alipompelekea wahyi wa kuijenga A-kaaba. Ibrahimu na mwanawe wakaitekeleza amri ya Mola wao wakaijenga Al-kaaba. Mwenyezi Mungu akamuamrisha Nabii Ibrahimu awaite watu kuja kuhiji na kufanya ibada katika nyumba yake hiyo tukufu. Ujenzi huu wa nyumba tukufu ya Mwenyezi Mungu na ibada tukufu ya Hijjah ndivyo vilivyoufanya mji wa Makkah kuwa ni mji mtakatifu. Hii ndio historia fupi ya kuasisiwa mji wa Makkah.

Makabila mengi yalipatikana kutokana na kizazi cha Ismail mwana wa Nabii Ibrahimu katika nchi ya Hijazi, kabila la Qurayshi ndilo lililokuwa mashuhuri zaidi. Baadhi ya makabila haya yalikuwa yakimuabudu Mwenyezi Mungu kupitia mafundisho ya dini ya Nabii Ibrahim- Amani ya Allah imshukie. Uongozi wa kidini na kibiashara ulitawaliwa na Maqurayshi kwa sababu ya ushujaa na ufasaha waliokuwa nao, sifa hizi ndizo zilizolipelekea kabila la Qurayshi kuyatawala makabila mengine yote. Mji wa Makkah na Maqurayshi walizidi kupata utukufu pale Mzee Qusway Bin Kilaab-babu wa nne wa Mtume aliposhika hatamu za uongozi wa mji wa Makkah. Mzee huyu alikuwa ni mtu mwenye busara, fikra na hekima. Alianzisha mpango mji, bunge ili watu wote wa Makkah waweze kukutana humo na kushauriana/kujadili mambo yao, pia aliijenga upya Al-Kaaba baada ya kuanza kuonyesha athari za kubomoka. Kadhalika alianzisha utaratibu wa kuwasaidia masikini kwa kuwapa chakula na maji. Baada ya kupita vizazi vingi, taratibu Maqurayshi walianza kuyatupa mafundisho ya dini ya Nabii Ibrahimu na kuanza kuyaabudu masanamu yaliyotengenezwa na mikono yao wenyewe. Ibada ya msanamu ilikuwa ni matokeo ya safari ya mmoja wa viongozi wa Maqurayshi alipokewenda Shamu na kuwakuta watu wa huko wakiyaabudia masanamu na akapendezwa na kuvutiwa na ibada hiyo. Akarejea Makkah na sanamu moja, akaliweka ndani ya Al-kaaba na kuanza kuliabudia. Watu wa Makkah kuona hivyo nao wakamuiga kiongozi wao, wakatengeneza masanamu yao wakayaweka ndani ya Al-kaaba na kuyaabudia na huo ukawa ndio mwanzo wa kuiacha na kuitupa mila ya Nabii Ibrahimu.
-----------------------------------------------------------------------------------------------

SOMO LA PILI
SOMO LA PILI
i) HALI YA KIDINI KATIKA BARA ARABU KABLA YA UISLAMU Kabla ya kudhihiri kwa Uislamu Bara arabu halikuwa na dini moja bali lilisheheni dini nyingi. Baadhi ya wakazi wake walikuwa wakifuata dini ya Nabii Musa nao ni mayahudi na wengine waliifuata dini ya Nabii Isa, nao ni Manasara. Mbali na hawa walikuwepo pia waliokuwa wakiyaabudia masanamu. Qur-ani Tukufu imeyataja baadhi ya masanamu yaliyofanywa miungu kama vile Laata,Uzzah, Yaghuuth, Yauuqa na Nasrah. Kadhalika lilikuwepo kundi dogo lililokuwa likifuata dini ya haki likimuabudu mola wa haki kupitia mafundisho yaliyoletwa na Nabii Ibrahimu kutoka kwa Mwenyezi mungu.
Mwenyezi Mungu Mtukufu alipompa utume Muhammad na kumpa kazi nzito na jukumu kubwa la kutangaza dini ya Kiislamu aliinuka na kuanza kuwalingania watu wamuabudu Mungu mmoja asiye na mshirika na waache kuyaabudu masanamu waliyoyatengeneza wao wenyewe. Jawabu la Maquraysh lilikuwa ni kumkadhibisha Mtume na kumpinga vikali sana. Isitoshe walimuadhibu adhabu kali sana kila aliyemuamini na kumfuata Mtume ili iwe ni onyo kwa wengine. Hawakukomea hapo tu bali waliwazuia watu kuonana na kumsikiliza Mtume lakini kwa sababu ya subira, jihadi, imani yake na msaada wa Mwenyezi Mungu alifanikiwa kuwashinda maadui wa Uislamu na kuieneza dini ya Mwenyezi Mungu miongoni mwa Waarabu na watu wa mataifa mengine.

ii) IBADA YA MASANAMU
Kabla ya Uislamu waarabu walizama mno katika ibada ya masanamu mpaka wakaijaza Al-Kaaba masanamu ambayo idadi yake ilifikia masanamu mia tatu na sitini (360). Kila kabila lilikuwa na sanamu lake pekee na kila kaya/familia ilikuwa na sanamu malum kwa ajili ya familia hiyo tu. Mtu alipotaka kusafiri, alilichukua safarini sanamu moja ilikufanikiwa safarini na walikuwa wakiyatakasa na kuyatukuza masanamu haya kiasi cha kuyatolea Qurubaani na dhabihu (sadaka za kuteketeza). Waarabu walipokuwa wakitaka ushauri katika mambo yao mfano ndoa, biashara au safari basi uliendea "Hubal" sanamu lililokuwa ndani ya Al-kaaba wakampa ngamia na dir-ham mia mshika kete ambazo moja ilikuwa imeandikwa juu yake maneno"Mungu wangu amenikataza" na ya pili "Mungu wangu ameniamrisha" ya tatu "Naam/Ndiyo" ya nne "Hapana". Jumla kete zilikuwa ni saba, mshika kete huzizungusha na kuzichanganya kisha akaitoa moja na kilichoandikwa juu yake ndio huwa amri iliyotoka kwa Mungu sanamu.

HALI YA KIDINI KATIKA BARA ARABU KABLA YA UISLAMUKabla ya kudhihiri kwa Uislamu Bara arabu halikuwa na dini moja bali lilisheheni dini nyingi. Baadhi ya wakazi wake walikuwa wakifuata dini ya Nabii Musa nao ni mayahudi na wengine waliifuata dini ya Nabii Isa, nao ni Manasara. Mbali na hawa walikuwepo pia waliokuwa wakiyaabudia masanamu. Qur-ani Tukufu imeyataja baadhi ya masanamu yaliyofanywa miungu kama vile Laata,Uzzah, Yaghuuth, Yauuqa na Nasrah. Kadhalika lilikuwepo kundi dogo lililokuwa likifuata dini ya haki likimuabudu mola wa haki kupitia mafundisho yaliyoletwa na Nabii Ibrahimu kutoka kwa Mwenyezi mungu.
Mwenyezi Mungu Mtukufu alipompa utume Muhammad na kumpa kazi nzito na jukumu kubwa la kutangaza dini ya Kiislamu aliinuka na kuanza kuwalingania watu wamuabudu Mungu mmoja asiye na mshirika na waache kuyaabudu masanamu waliyoyatengeneza wao wenyewe. Jawabu la Maquraysh lilikuwa ni kumkadhibisha Mtume na kumpinga vikali sana. Isitoshe walimuadhibu adhabu kali sana kila aliyemuamini na kumfuata Mtume ili iwe ni onyo kwa wengine. Hawakukomea hapo tu bali waliwazuia watu kuonana na kumsikiliza Mtume lakini kwa sababu ya subira, jihadi, imani yake na msaada wa Mwenyezi Mungu alifanikiwa kuwashinda maadui wa Uislamu na kuieneza dini ya Mwenyezi Mungu miongoni mwa Waarabu na watu wa mataifa mengine.

Kabla ya Uislamu waarabu walizama mno katika ibada ya masanamu mpaka wakaijaza Al-Kaaba masanamu ambayo idadi yake ilifikia masanamu mia tatu na sitini (360). Kila kabila lilikuwa na sanamu lake pekee na kila kaya/familia ilikuwa na sanamu malum kwa ajili ya familia hiyo tu. Mtu alipotaka kusafiri, alilichukua safarini sanamu moja ilikufanikiwa safarini na walikuwa wakiyatakasa na kuyatukuza masanamu haya kiasi cha kuyatolea Qurubaani na dhabihu (sadaka za kuteketeza). Waarabu walipokuwa wakitaka ushauri katika mambo yao mfano ndoa, biashara au safari basi uliendea "Hubal" sanamu lililokuwa ndani ya Al-kaaba wakampa ngamia na dir-ham mia mshika kete ambazo moja ilikuwa imeandikwa juu yake maneno"Mungu wangu amenikataza" na ya pili "Mungu wangu ameniamrisha" ya tatu "Naam/Ndiyo" ya nne "Hapana". Jumla kete zilikuwa ni saba, mshika kete huzizungusha na kuzichanganya kisha akaitoa moja na kilichoandikwa juu yake ndio huwa amri iliyotoka kwa Mungu sanamu

HALI YA KIJAMII NA TABIA ZA WAARABU
Tumeeleza huko nyuma kwamba yalipatikana makabila mengi ya kiarabu kutokana na kizazi cha Nabii Ismail. Kila kabila liliundwa kutokana na kaya/familia kadhaaa zilizojiunga pamoja. Kila kabila liliongozwa na kiongozi aliyekuwa mtu mzima anayeheshimika, kukubalika na kutiiwa na wote. Ukabila ulikuwa ndio sera ya kila kabila, na kila kabila lilikuwa tayari kuilinda sera yake hiyo ya ukabila dhidi ya uadui wa wote ule kutoka makabila mengine kwa gharama yoyote ile. Msimamo huu na sera hii ya ukabila ilisababisha mizozo, ugomvi na mapigano ya mara kwa mara baina ya makabila haya. Kugombea vyanzo vya maji, machungo na kujifakharisha kwa nasabu pia vilichochea kwa kiasi kikubwa mizozo na mapigano. Kama ambavyo watu hutofautiana katika vyeo/hadhi, kazi na hali za kimaisha, Waarabu pia waligawanyika katika matabaka yafuatayo:-
  1. Mabwana/Viongozi: hawa ndio waliokuwa na mamlaka juu ya wengine na hatamu za uongozi zilikuwa chini yao.
  2. Makuhani: hawa walikuwa ndio viongozi wa kidini wakiyatawalia mambo yote yanayohusu dini ikiwa ni pamoja na ibada, sherehe za kidini na mengineyo.
  3. Wafanyabiashara: hawa walijishughulisha na usambaji na uuzaji wa bidhaa mbalimbali ndani na nje ya maeneo yao.
  4. Wachungaji: hawa ndio waliokuwa wakijishughulisha na uchungaji wa wanyama na kazi ya kilimo kwa kiasi fulani.
Ama kwa upande wa kitabia,Waarabu za jahilia kama walivyo watu wa zama hizi walikuwa na tabia nzuri na nyingine mbaya. Miongoni mwa tabia njema walizokuwa nazo ni kama vile ukarimu, murua, ushujaa na utekelezaji wa ahadi. Tabia mbaya zilizoitawala jamii ile ni pamoja na ulevi, uchezaji wa kamari, ulaji riba na kuwazika watoto wa kike wakiwa hai kama ilivyoelezwa na Qur-ani:
"NA MTOTO MWANAMKE ALIYEZIKWA HALI YAKUWA YU HAI ATAKAPOULIZWA. KWA MAKOSA GANI ALIUAWA. (81:8-9)

SOMO LA TATU
i/NASABU YA MTUME KUUMENI KWAKE
Nasabu ya Bwana Mtume – Allah amrehemu na kumshushia amani – kwa upande wa baba yake ni kama ifuatavyo:-
Yeye ni Muhammad Bin Abdillah Bin Abdil – Mutwalib Bin Haashim Bin Abdi Manaf Bin Qusway Bin Kilaab Bin Murrah Bin Kaab Bin Luayyi Bin Ghaalib Bin Fihr Bin Maalik Bin Nadhr Bin Kinaanah Bin Khuzaymah Bin Mudrikata Bin Ilyaas Bin Mudhwar Bin Nizaar Bin Maad Bin Adnaan. Huu Adnaan ni katika kizazi cha Nabii Ismail Bin Ibrahim – Amani iwe juu yao.

ii/NASABU YA MTUME KUKENI KWAKE
Nasabu yake Bwana Mtume – Allah amrehemu na kumshushia amani – kwa upande wa mama yake:-
Yeye ni Muhammad Bin Aaminah Bint Wahab Bin Abdi Manaf Bin Zuhrah Bin Hakiym. Huyu Mzee Hakiym ndiye Kilaab ambaye ni babu wa tano wa Mtume kwa upande wa baba yake.
Tumekwishaeleza huko nyuma kwamba huyu Mzee Qusway ambaye ni babu wa nne katika mlolongo wa babu zake Mtume ndiye aliyeweka mpango wa mji wa Makkah na akawaunganisha pamoja Waarabu kwa kuondosha ukabila.
Baada ya kifo cha Mzee Qusway, hatamu za uongozi wa mji wa Makkah zilishikwa na babu wa pili wa Mtume Mzee Haashim. Huyu alikuwa tajiri na ndiye aliyeasisi mfumo wa biashara za Kusi na kaskazi kama ulivyoelezwa na Qur-ani:-
"ILI KUWAFANYA MAKURESHI WAENDELEE. WAENDELEE NA SAFARI ZAO ZA WAKATI WA KUSI (kwenda yaman) NA WAKATI WA KASKAZI (kwenda Shamu, ndio maana tukajaalia jeshi la ndovu kushindwa) (102:1-2)
Pia Mzee huyu ndiye aliyesimamia usambazaji wa maji na chakula kwa wageni wote wanaokuja kufanya ibada katika Al-kaaba na hili linaashiria ukarimu walikuwa nao Waarabu. Naye ndiye mtu wa mwanzo aliyeanzisha uokaji na usambaji wa mikate katika mji wa Makkah na hili linaonyesha ni jinsi gani alivyowajibika kwa jamii iliyompa dhamana ya uongozi.
Mwenyezi Mungu aliitakasa nasabu ya Mtume kutokana na uchafu wa kijahilia. Mababa zake wote walikuwa ni watu watukufu na viongozi kama ambavyo mamama zake pia walikuwa ni wanawake waungwana,watakasifu wasio na uchafu wowote.
Lifuatalo ni jedwali na kielelezo kinachoonyesha nasabu ya Mtume kuanzia kwa babu wake wa nne Mzee Qusway. Jedwali hili litatusaidia kuelewa koo za Maqureshi huko mbele.















 


 


 
 

No comments:

Post a Comment