SPORTS


Jackie Robinson shoes: Carl Crawford warned by MLB, might get fined for wearing them

 

Apparently, it does matter if your shoes are blue and white. It matters to Major League Baseball, which warned Los Angeles Dodgers slugger Carl Crawford to never again wear the special edition Jackie Robinson cleats he wore Monday.
Crawford was among several major leaguers who received two pair of the Nike Air Jordan/Jumpman/Swingman/whatever shoes — one in Brooklyn Dodgers blue, the other in white — and wore one of each on the 66th anniversary of Robinson breaking the modern color barrier in the majors. What Crawford did was a no-no, ESPN's Mark Saxon reports:


Leo ni vita,Bayern Munich na Barcelona

 23 Aprili, 2013 - Saa 05:10 GMT

Messi akishangilia moja ya mabao yake na David Villa
Vita kusaka tiketi ya kusafiri kwenda jijini London kwenye mchezo wa fainali wa klabu bingwa barani Ulaya inaanza usiku huu kati ya Mabingwa wa soka nchini Ujerumani dhidi ya inayotajwa kuwa timu bora kwa vilabu vya soka duniani kwa wakati huu FC Barcelona.
Kocha wa Bayern Munich, Jupp Heynckes amesema haogopeshwi na urejeo wa nyota wa Barcelona, Lionel Messi kuelekea mchezo huo wa kwanza wa nusu fainali ya klabu bingwa barani Ulaya.
Messi hajacheza mchezo wowote wa Barcelona toka alipoingia kama mchezaji wa akiba na kuisaidia timu yake kufuzu nusu fainal katika mchezo robo fainali dhidi ya Paris St-Germain ya Ufaransa. Lakini kuna kila dalili Muanjetina huyo mwenye umri wa miaka 25 ambaye ndiye mchezaji bora wa dunia kwa sasa,akajumuishwa kwenye kikosi cha Barcelona kwenye mchezo wa usiku wa leo.
Mwezi uliopita Messi aliweka rekodi kwenye ligi ya Hispania kwa kuwa mchezaji aliyezifunga timu zote zinazoshiriki ligi kuu nchini humo maarufu kama La Liga kwa misimu miwili mfululizo.
Barcelona inapambana kutaka kutwaa taji la tatu la klabu bingwa barani Ulaya ndani ya miaka mitano,Huku Bayern Munich ambao msimu ujao watakuwa chini ya aliyekuwa kocha wa Barcelona, Pep Guardiola, wao wanapambana kutafuta nafasi ya kucheza fainali yao ya tatu ndani ya miaka minne.
mashabiki wa Bayern Munich
Kocha wa Bayern Munich, Jupp Heynckes ambaye aliwahi kuwafundisha mahasimu wa Barcelona, Real Madrid amesema licha ya kumheshimu mrithi wake wa kiti cha ukocha kwenye timu hiyo lakini hajaomba ushauri wowote kutoka kwa Guardiola na amejiandaa kwa kila namna kuhakikisha anaifunga Barcelona usiku huu. Aliongeza kwa kusema anaijua vizuri sana timu yake kuliko mtu yeyote na anafahamu soka ya Hispania na Barcelona wenyewe kwa undani mkubwa.
Wakati Barca wakiwa hawajaweka wazi kama watamuanzisha Messi au la, Baadhi ya wachezaji wa Barcelona akiwemo Xavi Hernandez alinukuliwa siku ya jumatatu akisema, kombe la ligi kuu nchini Hispania, La Liga lina umuhimu mkubwa kuliko klabu bingwa barani Ulaya.
Mechi hiyo itachezwa kwenye uwanja wa Allianz Arena mjini Munich nchini Ujerumani,majira ya saa nne kasorobo usiku kwa saa Afrika Mashariki.



FA Uingereza yamfungulia mashtaka Suarez

 23 Aprili, 2013 - Saa 01:45 GMT

Suarez akimng`ata Ivanovic uwanjani
Chama cha soka nchini Uingereza, FA kimenuia kumpa adhabu kali mshambuliaji wa Liverpool Luis Suarez kwa kitendo chake cha kumng'ata beki wa Chelsea Branislav Ivanovic katika mchezo wa jumapili baina ya Liverpool na Chelsea,mchezo uliomalizika kwa sare ya 2-2.
FA imesema mwamuzi wa mchezo huo hakukiona kitendo hicho uwanjani lakini marejeo ya picha za mchezo huo zilionyesha Suarez alimng'ata Ivanovic,kitendo ambacho kinachukuliwa kama vurugu mchezoni na adhabu yake ni kufungiwa mechi tatu lakini adhabu hiyo haitoshi kwa tukio alilolifanya Suarez.
Suarez amepewa muda wa mpaka saa 12 jioni jumanne ya April 23, awe amekubali au kukataa kosa hilo kabla ya tume ya kudhibiti maadili haijakutana hapo siku ya jumatano kutoa hukumu stahili kwa kosa hilo.
Mwenyewe Suarez aliisha kiri kufanya kosa hilo na kumuomba Ivanovic msamaha kwa njia ya simu na kuwaomba mashabiki wa soka wamsamehe kwa kosa hilo.
Klabu yake ya Liverpool imempa adhabu ya kumpiga faini mchezaji huyo wa kimataifa wa Uruguay.
Mwaka 2010, Suarez wakati akiichezea Ajax ya Uholanzi alimng'ata begani kiungo wa PSV Eindhoven, Otman Bakkal na kufungiwa mechi saba na chama cha soka nchini Uholanzi kwa kosa hilo.
Itakumbukwa Suarez tayari amekwishawahi kufungiwa kutocheza mechi nane za mashindano nchini Uingereza na faini ya paundi elfu 40 kwa kosa la kumtolea lugha ya kibaguzi beki wa Manchester United Patrice Evra mwaka 2011.


No comments:

Post a Comment