News


 June 1, 2013
Death toll in apartment explosion in upscale Manila district 
rises to six
The death toll from a powerful explosion that ripped through an upscale apartment complex in the Philippine capital Manila has risen to six, including the crew of a passing delivery van that was hit by debris.
Death toll in apartment explosion in upscale Manila district rises to six
Member of the presidential security group looks at a delivery van crushed by debris after a powerful explosion that rocked Taguig city Photo: REUTERS
The explosion punched a large hole in the wall of the apartment building and sent concrete chunks flying onto the street below, which was teeming with pedestrians. Three people in the van were crushed to death.
The Office of Civil defence said three more bodies were recovered at the Serendra building, a plush condominium complex surrounded by restaurants and shops in Taguig city in metropolitan Manila.
Five others, including a nine-year-old, were injured.
Authorities were initially looking into a gas supply issue, and residents were kept out of other buildings as officials assessed the supply maintenance.
A telephone operator at the Taguig city police station, who declined to give her name because she was not authorised to speak to the media, said the explosion came from an appliance and was not caused by a bomb.

June 1, 2013
Chuck Hagel accuses China of 'cyber intrusions' on US
US Defense Secretary Chuck Hagel has accused China of waging cyber espionage against the United States, stepping up pressure on Beijing over the issue ahead of a key bilateral summit.
Chuck Hagel: Chuck Hagel accuses China of 'cyber intrusions' on US
Chuck Hagel accuses China of 'cyber intrusions' on US  Photo: AP
Speaking at a Singapore security forum attended by senior Chinese military officials, the Pentagon chief pointedly blamed the Chinese government and armed forces for repeated intrusions into sensitive US information systems.
"The United States has expressed our concerns about the growing threat of cyber intrusions, some of which appear to be tied to the Chinese government and military," he told an annual conference known as the Shangri-La Dialogue.
Hagel pressed Beijing to adhere to "international norms of responsible behaviour in cyberspace", while acknowledging that the establishment of a joint cyber security working group was a positive step in fostering US-China dialogue on such issues.
The Singapore forum came ahead of the June 7-8 meeting between US President Barack Obama and his Chinese counterpart Xi Jinping in California, the two leaders' first meeting since Xi took office in March.
China's delegation to the Singapore meeting was led by Lieutenant General Qi Jianguo, a deputy chief of the general staff of the People's Liberation Army.

 May 29, 2013

Nawaz Sharif 'to invite Taliban commanders to peace talks'

Pakistan's prime minister-elect Nawaz Sharif is to invite Taliban commanders to join peace talks, after he is formally sworn in next week, sources close to the incoming government have confirmed.
Nawaz Sharif 'to invite Taliban commanders to peace talks'
Nawaz Sharif will be appointed as prime minister next week Photo: EPA
Mr Sharif, who will become the first leader in Pakistan's history to serve three terms as prime minister when he is formally appointed next week, has long supported dialogue with the militants who have waged war on Islamabad since former dictator General Musharraf backed the United States-led invasion of Afghanistan in 2001.
Since then a number of peace deals have been struck with insurgency leaders, including one where Taliban leaders were paid large amounts of cash in 'reparations' which were paid in turn to al-Qaeda. All of the deals foundered in acrimony but heightened tensions between Pakistan and the United States.
Mr Sharif's Pakistan Muslim League (N) party is understood to be wary of repeating mistakes made in the earlier 'peace deals' but believes the conflict can only be resolved through dialogue.
Shortly after his party's convincing victory in the Pakistan National Assembly elections, he told supporters :"All options should be tried, and guns and bullets are not a solution to all problems … Why shouldn't we sit and talk and engage in dialogue?" he said.
Next week however he is expected to intensify peace efforts by calling a 'grand jirga' of tribal elders to open peace talks with Taliban commanders in a process brokered by the Jamiat ul Islami (F), a conservative Islamic party which is set to join Mr Nawaz's government. Jan Achakzai, spokesman for the JUI (F)'s leader Maulana Fazl-ur Rahman confirmed his party's role in broking the new peace process, which he said would also involve representatives of the country's army and the Khyber Pukhtunkhwa provincial government which will be lead by Imran Khan's PTI party.

Ubaguzi kwa Waislamu waongezeka

 25 Mei, 2013

    Shirika la Uingereza la mchanganyiko wa dini mbali-mbali linasema jamii zimeingiwa na uoga tangu kuchinjwa kwa mwanajeshi wa Uingereza na Waislamu wenye siasa kali katika barabara ya mjini London.
    Muislamu mjini London
    Shirika hilo, Faith Matters, limesema mashambulio yameongezeka sana tangu kuuwawa kwa mwanajeshi huyo siku ya Jumatano.
    Linasema limearifiwa visa zaidi ya 162 vya ubaguzi dhidi ya Waislamu katika siku mbili - kutoka misikiti kushambuliwa hadi matusi.
    Viongozi wa Kiislamu wa Uingereza wamelaani vikali mauaji ya mwanajeshi huyo.

     

    Nigeria kuwaachiliwa wanawake washukiwa


    Wapiganaji wa Boko Rama wamewateka nyara wanawake na wasichana
    Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan, ameamuru kuachiliwa kwa wanawake wote waliokamatwa kwa kuhusishwa na vitendo vya kigaiidi. Hii ni kwa mujibu wa taarifa kutoka wizara ya ulinzi.
    Kulingana na wizara hiyo, uamuzi huo ulilenga kuimarisha juhudi za amani nchini Nigeria.
    Jeshi linaendesha operesheni katika majimbo matatu ambako sheria ya hali ya hatari ilitangazwa wiki jana ili kuwezesha jeshi kupambana vilivyo na wapiganaji wa kiisilamu wa Boko Haram.
    Kundi hilo lilisema kuwa halitawaachilia wanawake na watoto waliowateka nyara ikiwa serikali haitafanya mazungumzo nao
    Zaidi ya watu 2,000 wamefariki nchini Nigeria katika mashambulizi yaliyofanywa na Boko Haram tangu mwaka 2009 wakitaka kuundwa kwa jimbo litakalofuata sheria za kiisilamu.
    Mapema mwezi huu kundi hilo lilitangaza kuwateka nyara wanawake na wasichana wadogo kulipiza kisasi hatua ya jeshi kuwakamata wake za wanamgambo hao.
    Wapiganaji hao walisema kuwa wanafanya wanawake hao kuwa watumishi wao.
    Wizara ya ulinzi ilisema kuwa wanawake kadhaa waliokamatwa kama washukiwa wa ugaidi , watakabidhiwa kwa polisi ili kupewa mafunzo ya kurekebisha tabia yao kabla ya kuachiliwa.
    Duru zinasema kuwa uamuzi wa rais Jonathan, haujaonda fursa ya kufanyika mazungumzo kati ya serikali na wapiganaji wa Boko Haram, licha ya kuazisha operesheini ya kijeshi dhidi ya wapiganaji hao.
    Rais Goodluck, alitangaza sheria ya kutotoka nje katika majimbo matatu ya Kaskazini Mashariki, Borno, Yobe na Adamawa, ambako Boko Haram lina ngome zake kuu.
    Wanajeshi 2,000, walipelekwa katika maeneo hayo wiki jana, ikiwa ni moja ya operesheni kubwa zaidi ya kijeshi dhidi ya Boko Haram kuwahi kushuhudiwa.
    Jeshi limesema kuwa pia limesema lilitumia ndege za kivita kushambulia ngome za kundi hilo.
    Waziri wa mambo ya nje nchini Marekani John Kerry, ameitaka serikali ya Nigeria kuhakikisha kuwa jeshi halikiuki haki za binadamau wakati likiendesha kampeini hiyo dhidi ya Boko Haram.
    Bwana Kerry alisema kuwa kuna ushahidi wa kutosha kuonyesha jeshi limekiuka haki za binadamu.

     

    Wapiganaji wa Boko Haram wakamatwa Maiduguri

     22 Mei, 2013


    Jeshi linasema wapiganaji kadhaa wametoroka na kuingia katikla nchi jirani za Chad, Niger na Cameroon
    Takriban wapiganaji 120 wamekamatwa katika mji wa Maiduguri, eneo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria wakati walipokuwa wanaandaa mazishi ya kamanda wao. Hii ni kwa mujibu wa msemaji wa jeshi.
    Jeshi pia limeteka maeneo matano kutoka kwa wapiganaji hao.

    Hata hivyo hakuna taarifa zengine kuthibitisha madai ya wanajeshi hao.
    Rais Goodluck Jonathan, alitangaza sheria ya hali ya hatari katika majimbo matatu, Mashariki mwa Nigeria ili kutuliza hali ambayo imekuwa ikivurugwa na wapiganaji wa Boko Haram.
    Kundi hilo limekuwa likifanya mashambulizi na mauaji ya kupangwa tangu mwaka 2009, wakisema wanataka kuunda jimbo la kiisilamu nchini humo.
    Kundi lengine la kiisilamu liitwalo Ansaru, lilijiunga na harakati za Boko Haram mwaka 2012 na limekuwa likiwateka nyara watalii.
    Maafisa wanasema kuwa takriban watu, 2,000 wametoroka makwao na kuingia nchi jirani ya Niger, wakati wengine wakivuka na kuingia Cameroon,tangu jeshi kuanza operesheni yake dhidi ya wapiganaji hao katika majimbo ya Borno, Adamawa na Yobe wiki jana.
    Wanajeshi 2,000, walipelekwa katike eneo hilo wiki jana katika operesheni kubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa dhidi ya wapiganaji hao wa kiisilamu.
    Jeshi limesema kuwa pia linatuma wanajeshi wengine 1,000 Adamawa .
    Wapiganaji wanaotoroka na kuingia nchi jirani za Chad na Niger wanadhibitiwa kulingana na Chris Olukolade.
    "wanajeshi pia walisema waliona makaburi yanayoaminika kuwa ya wapiganaji waliozikwa kwa haraka huku wengine wakiwa njiai wakitoroka operesheni ya jeshi dhidi yao.''
    Brigedia Gen Olukolade, alisema takriban wapiganaji 120 waliokamatwa wanahojiwa na kufikisha 200 idadi ya wale waliokamatwa na jeshi tangu wiki jana.
    Wanamgambo walikamatwa huku wakijiandaa kwa mazishi ya kamanda wao aliyeuawa kwenye opereshi hiyo.
    Jeshi hilo limeweza kuteka miji mitano na viji kutoka kwa wanamgambo hao katika maeneo ya mashinani katika jimbo la Borno, na kuaharibu kambi zote za wapiganaji hao.
    Wiki jana Jeshi lilisema kuwa lilishambulia ngome za wapiganaji hao katika mbuga ya wanyama ya Sambisa Kusini mwa Maiduguri.
    Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani, John Kerry, ametaka jeshi la Nigeria kujizuia na kutokiuka haki za binadamu huku likiwasaka wapiganaji hao.

    MLINZI WA BAR ACHINJWA KIKATILI NA MAJAMBAZI USIKU WA KUAMKIA LEO



    Mlinzi wa baa ya Darajani Stop Over iliyo kando kando ya barabara kuu ya Morogoro Dar es salaam jirani na daraja la Mzambarauni  Bw Mika Athumani amechinjwa na majambazi usiku wa kuamkia leo.


    Habari zilizopatikana eneo la tukio zilidai kwamba majambazi hayo yalivamia baa hiyo iliyojitenga usiku wa manane na kumvamia mlinzi huyo na kumchinka kama kuku na baadae kuvunja baa hiyo na kuimba vitu mbali mbali.

    Mwili wa marehemu ukiwa ndani ya gari, la polisi kufuatia mwili huo kutenganiswa vibande viwili..



    Sehemu aliyochinjiwa mlinzi huyo aliyefahamika kwa jina Mika Athumani.
    Akihojiwa na mwandishi wetu,  mmiliki wa baa hiyo Bw Salvatory Mushi alidai kwamba majambazi hao walimvamia mlinzi wake na kumchinja na baadae walivunja Counter ya baa hiyo pamoja na duka ililipojirani na baa hiyo na kuiba vitu mbali mbali.
     

    Alipoulizwa kwamba kuna taarifa zinadai kwamba mlinzi huyo alikutwa akiwa amelala Bw Mushi alisema"  inawezekana lakini hakuna mtu mwenye uhakika na jambo hilo kwani sote hatukuwepo,wakti tukio hilo linatokea"
    Mwananachi akishuhudia damu ya mlinzi huyo kwa hudhuni
    Baskeli ya Mlizni huyo ikiwa imetapakaa damu ambapo inadaiwa mlinzi huyo alikuwa amelala kwenye eneo hilo
    Redio ambayo majambazi hayo waliiangusha nje ya baa hiyo
    Majaira ya saa 12 asubuhi ya leo wananchi walishuhudia maduka mawili ya baa hiyo yakiwa wazi huku mwili wa mlizni huyo umekutwa upande wa baa ukiwa umechinjwa na kutenganishwa kichwa na mwili
    Umati wa watu ukishuhudia tukio hilo muda mfupi uliopita
    Gali la polisi likiondoka eneo la tukio na mwili wa marehemu
    Wananchi nao waliondoka eneo hilo la tukio
    Mmiliki wa baa hiyo Bw Salvatory Mushi akihojiwa na waandishi wa habari eneo la tukio

    Majirani wa eneo hilo wakihojiwa na waandishi wa habari
    Baadhi ya watu waliokuwepo eneo hilo la tukio walidai kwamba mlinzi huyo alikuwa amelala hivyo majambazi hayo yalimvamia na kumpora siraha zake na kishi kumchinja shingoni..
    Mwandishi wetu alishuhudia mtoto wa marehemu pamoja na mjukuu wa marehemu wakiangua vilio eneo la tuko baada ya kuuona mwili wa mazazi wao aliyeuwawa kikatili baadae wote wawili walipanda gari la polisi na kuondoka nao.

    ELIMU YA SHULE ZA MSINGI ITAKUWA NI MIAKA 10 BADALA YA 7

    RASIMU ya Sera ya Elimu na Mafunzo nchini inapendekeza kuunganisha elimu ya msingi na sekondari ya kawaida ya sasa ili kuunda elimu-msingi itakayotolewa kwa kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2018, imefahamika. 
    Rasimu ya kwanza ya Sera hiyo imeshakamilika na sasa wadau mbalimbali wanatoa mapendekezo yao kuiboresha, kabla ya kupelekwa bungeni ili kutungiwa sheria.
    Aidha, mikakati hiyo itakayotekelezwa ni kuhuisha muundo na utaratibu mpya wa elimu na mafunzo kwa kuhakikisha kila mtoto mwenye umri wa miaka mitatu na mitano anapitia elimu ya awali kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja kabla ya kujiunga na elimu-msingi.
    Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo alithibitisha kwa gazeti hili wiki hii mjini hapa kuhusu kukamilika kwa rasimu ya kwanza ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2013.
    “Ni kweli Sera hiyo imekamilika baada ya kuandaliwa kwa miaka mitatu. Imepita kwa wadau mbalimbali, mashuleni, vyuoni na katika taasisi mbalimbali nchini ambao wametoa maoni yao. “Jumapili (kesho) tunatarajia kuwa waheshimiwa wabunge nao watapata fursa ya kuijadili na kutoa maoni yao katika semina iliyoandaliwa maalumu kwao,” alisema Mulugo katika Viwanja vya Bunge.
    Alisema baada ya maoni hao ya wabunge, watapeleka Rasimu hiyo kwa mamlaka husika kwa ajili ya andiko la mwisho kabla ya kupelekwa katika Bunge lijalo ili itungwe sheria kuhusu Sera ya Elimu na Mafunzo.
    Hata hivyo, semina hiyo huenda isifanyike kesho kutokana na kuingiliana na ratiba nyingine, kwani wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) watakuwa na mkutano na Mwenyekiti wao wa Taifa, Rais Jakaya Kikwete, kwenye Ukumbi wa White House mjini hapa.
    Wiki moja iliyopita, wakati akiongoza kikao, Spika wa Bunge, Anne Makinda aliwaambia wabunge kuwa makabrasha waliyokuwa wakipewa na wahudumu ni kuhusu Sera ya Elimu na hivyo waende wakayasome, kwani kuna siku wataijadili.
    Kwa mujibu wa rasimu, mambo mengine yanayotarajiwa kutekelezwa na Sera ni kuhuisha mitaala ya sasa ya elimu ili ikidhi muundo mpya wa elimu na mafunzo, kuhuisha sheria na taratibu mbalimbali za utoaji elimu ili ziendane na muundo mpya wa elimu-msingi.
    Kuimarisha mfumo wa usimamizi, ithibati na udhibiti wa utoaji wa elimu na mafunzo katika ngazi mbalimbali ili kukidhi malengo na muundo mpya wa elimu-msingi.
    Nyingine ni kuongeza ubora wa miundombinu katika shule za sasa za msingi ili kukidhi mahitaji na malengo ya elimu-msingi ikiwa ni pamoja na kuongeza madarasa ya elimu-msingi katika kila shule ya msingi ya sasa, kujenga maabara za sayansi na maktaba katika kila shule ya elimu-msingi.
    “Kutenga rasilimali fedha za kutosha kwa ajili ya nyenzo, vifaa na zana za kufundishia na kujifunzia, vitabu vya kiada na ziada, maandiko, machapisho ya maktaba pamoja na vifaa vya maabara,” ilieleza rasimi hiyo ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Kuimarisha matumizi ya lugha za Kiswahili na Kiingereza katika ngazi ya elimu – msingi kama lugha za kujifunzia na kuwasiliana.
    Kuweka utaratibu utakaohakikisha kuwa wanafunzi wanaomaliza elimu na mafunzo ngazi husika kwa ufanisi na wale wanaokatisha masomo au mafunzo yao kwa sababu mbalimbali, wanaendelea na kuhitimu masomo au mafunzo yao katika mfumo rasmi wa elimu na mafunzo. Jambo jingine litakalotekelezwa ni kutoa elimu kwa umma kuhusu madhumuni, malengo na matarajio ya Sera mpya ya Elimu na Mafunzo.
    Rasimu ilieleza kuwa mambo chanya yanayotarajiwa kupatikana baada ya mkakati kutekelezwa ni kuwepo kwa elimu ya awali ya lazima kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja kabla ya kujiunga na elimu msingi, kuwepo kwa elimu msingi ya miaka 10 kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne cha sasa kwa watoto wote wenye rika la kwenda shule.
    Matokeo mengine ni kuwepo kwa mfumo nyumbufu, miundo na taratibu za kujiendeleza katika mikondo anuai ya kitaalamu na kitaaluma, kuwepo kwa elimu na mafunzo yenye viwango, ubora na sifa zinazotambulika kitaifa, kikanda na kimataifa.
    “Kuwepo kwa fursa mbalimbali za elimu na mafunzo zinazokidhi mahitaji ya wananchi na ya nchi kiuchumi, kijamii, kisayansi na kiteknolojia.
    “Kuwepo kwa ugharimiaji endelevu wa elimu na mafunzo na kuwepo kwa mfumo wa elimu na mafunzo unaozingatia masuala mtambuka,” ilifafanua Rasimu ya Sera ya Elimu na Mafunzo.
    Kuhusu elimu ya awali, ilieleza kuwa mkakati ni kuweka vigezo, viwango na taratibu ili elimu ya awali iwe ya lazima na itolewe katika kila shule ya elimu – msingi, na kuwa sheria, miongozo na taratibu kuhusu elimu hiyo lazima kuwekwa na kutekelezwa ifikapo mwaka 2018.
    Katika elimu msingi, ni kuwa ya lazima kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne, na kutolewa kwa miaka 10 na umri wa kuanza darasa la kwanza kuwa kati ya miaka minne hadi sita kulingana na uwezo wa mtoto kumudu masomo katika ngazi husika.
    Shabaha katika eneo hili ni sheria na miongozo kuhusu elimu-msingi kuwekwa na kutekelezwa ifikapo mwaka 2016, mpango wa utekelezaji wa utoaji wa elimu-msingi kuwepo ifikapo mwaka 2018 na elimu-msingi kutolewa ifikapo 2018.
    Kwa mujibu wa dibaji ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa, Sera mpya imeandaliwa na Serikali kwa kushirikiana na wadau ikitilia maanani mafanikio yaliyoletwa na Sera zilizotangulia na kulifanya Taifa kupiga hatua katika nyanja za elimu na mafunzo.
     
    “Sera kuu zilikuwa ni Sera ya Elimu na Mafunzo 1995, Sera ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo 1996 na Sera ya Taifa ya Elimu ya Juu 1999 ambazo zilitekelewa sambamba na sera nyingine ambazo zinaigusa sekta ya elimu na mafunzo kama vile Sera ya Sayansi na Teknolojia 1996, Sera ya Habari na Utangazaji 2003, Sera ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na ya Binafsi 2009 pamoja na nyingine za aina hiyo,” alisema Dk Kawambwa.

    BREAKING NEWS: KANISA KATOLIKI LALIPULIWA NA BOMU JIJINI ARUSHA WAKATI MISA IKIENDELEA


    Taarifa  zilizotufikia  hivi  punde  ni  kwamba  bomu  limelipuka  katika  kanisa  katoliki, parokia  mpya  ya Olasisi  iliyokuwa  inazinduliwa  leo  jijini  arusha.....


    Bomu  hilo  limelipuka  wakati  waumini  wa  kanisa  hilo  wa  wakijiandaa  na  misa  ya  uzinduzi  wa  parokia  hiyo....
     
    Mpaka  sasa  haijajulikana  idadi  kamili  ya  watu  waliojeruhiwa  ama  kupoteza  maisha  lakini taarifa  za  awali  zinasema  kuwa  baadhi  ya  majeruhi  wamekimbizwa  hospitali

    Chanzo  cha  mlipuko  huo  inasemekana   kuwa  kuna  gari  ndogo  ilifika  kanisani  hapo  na  kusimama....


    Baadae  alishuka  mtu  aliyekuwa  amevalia  vazi  mithili  ya  kanzu  na  kurusha  kitu  kuelekea  kanisani  ambacho  ndicho  kilichosababisha  mlipuko  huo..


    Mgeni rasmi   katika  uzinduzi   huo  alikuwa  ni   balozi wa Vatican nchini Tanzania.Yupo  baada  ya kunusurika  katika  mlipuko huo

    Hizi ni taarifa za awali tu. Taarifa kamili itawekwa itakapopatikana. Tafadhali endelea kusikiliza Redio Maria Tanzania (inasikika pia online muda huu wakiwa wanatangaza kuhusu tukio hili )

     

    JESHI LA TANZANIA LIMESHATUA CONGO.....WAASI WA M23 WAANZA KUHAHA KWA KUJIKOSHA KWA WANANCHI


    Kwa mujibu wa mwandishi aliye na waasi  wa  m23, Diana Katabarwa kwenye Blog yake  anamnukuu kiongozi wa kisiasa wa M23  Mr. Bisimwa akiwambia wakazi wa North Kivu kuwa majeshi ya Tanzania na South Africa nimajeshi dhalimu yaliyo jaa rushwa na hayawezi kuibadili Congo....


    Bisimwa anadai  kwamba  majeshi  ya  Tanzania  yamekuja kuiba mali na kumsaidia KABILA awatawale   hali  itakayosababisha   jeshi lake la FDLR na waasi wa MAI MAI wapewa nafasi ya kuwa pora mali zao na kuwabaka wake zao na watoto....

    Mbali  na  hayo,  bwana Busimwa anadai kinyume na taarifa zilivyo , kikosi cha jeshi la Tanzania kikiwa na askari 450 kimesha ingia mashariki ya CONGO kwenye mji wa UVIRA SOUTH KIVU huku Kamanda wao (TPDF) akiwa mjini Goma. 



    Kikosi cha jeshi la SOUTH AFRICA kiko mita 20 kutoka waasi walipo kwenye mji wa MUNGI nje kidogo ya GOMA. 


    Pia aliwaeleza wananchi hao kuwa kuna makomandoo 30 wa jeshi la Ufaransa ambao wako mjini GOMA na  wamefikia Linda Hotel...


    BUSIMWA alidai wafaransa ndio walisimamia mauaji ya kimbari ya Rwanda ,kwa hiyo kuwepo kwao ni ishara mbaya kwa wakazi wa mashariki ya CONGO ambao wengi ni watusi.

    David Cameron: "Somalia imepiga hatua"

     7 Mei, 2013 - Saa 12:39 GMT


    Waziri Mkuu David Cameron asema Somalia imepiga hatua
    Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron amesema kuwa Somalia "imepiga hatua kubwa" katika kumaliza fujo na machafuko yaliodumu kwa zaidi ya miongo miwili.

    Bwana Cameron ni mwenyeji wa mkutano wa kutafuta amani ya kudumu nchini Somalia.
    Mkutano huo unalengo la kumsaidia Rais Hassan Sheikh Mohamud aweze kuijenga tena upya Somalia.
    Somalia inahesabiwa kuwa miongoni mwa mataifa yalioanguka na ambayo imekuwa ikihangaishwa na magaidi wa Al shabaab, uharamia na ukame ulioitikisa mwaka kati ya 2010 hadi 2012.
    Rais Mohamud wa Somalia amesema serikali yake itafaulu kuidhibiti nchi nzima na kukabiliana na utovu wa usalama ifikapo mwaka 2015.
    Mkutano huo utajikita zaidi katika masuala ya kujenga upya vikosi vya ulinzi na kukabiliana na ubakaji ambalo ni suala linalooonekana kama mwiko.
    Takriban watu saba waliuawa katika mlipuko wa bomu kwenye gari uliotokea katika mji mkuu Mogadishu siku ya Jumapili. Kundi la Al - Shabab ambalo lina mafungamano na Al - Qaeda linadai kuhusika na shambulio hilo.
    Mkutano huo ambao utakua chini ya uenyekiti wa Bw. Cameron na rais wa Somalia Hassan Sheikh Mahamoud unafuatia mkutano kama huo uliofanyika London na jijini Istanbul nchini uturuki mwaka jana, huku wasiwasi ukiongezeka katika jumuiya ya kimataifa kwamba Somalia imegeuka hifadhi ya wanamgambo wenye mahusiano na al Qaeda.
    "Ninamatumaini kwamba, wote tunaweza kuafikiana kuhusu mpango wa usalama wa muda mrefu, ambao utamaliza vitisho vya Al Shabab moja kwa moja," alisema Bw. Cameron.
    "Pia ninamatumaini tutaboresha uwazi na uwajibikaji ili watu wafahamu wapi rasilimali zinakwenda. Pia tunahitaji kuendelea na mchakato wa kulijenga taifa la Somalia, ikiwemo mikoa yote ya Somalia na nchi jirani hali kadhalika."
    Mchambuzi wa masuala ya Somalia wa BBC, Mary Harper anasema, kumekuwa na mabadiliko ya ghafla nchini humo katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.
    Kuna serikali mpya, ya kwanza katika kipindi cha zaidi ya miongo miwili kutambuliwa na Marekani, Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na wadau wengine muhimu, anasema.

    Waziri Mkuu David Cameron akiwa na Rais Hassan Sheikh wa Somalia, mjini London
    Akina mama katika mkutano wa Msatakabal wa Somalia mwaka 2012 mjini London.
    Al - Shabab imepoteza udhibiti wa miji muhimu, mashambulizi ya maharamia nje ya pwani ya Somalia yamepungua sana pamoja na ukame, ambao Umoja wa Mataifa unakadiria kwamba, ulisababisha vifo vya takriban watu 260,000 sasa umemalizika.
    Hata hivyo, changamoto kubwa zimebakia, ambapo Al - Shabab bado wana uwezo wa kushambulia na serikali inategemea askari wapatao 18,000 tu wa Umoja wa Afrika (AU), kwa ajili ya kulinda usalama.
    Somalia pia imegawanyika katika maeneo madogo ya mikoa inayojitawala, mingi ikiwa haipatani na serikali kuu.
    Mkoa uliojitenga wa Somaliland na mkoa wenye mamlaka ya kati wa Puntland wamesema hawatahudhuria mkutano huo.
    Mkutano utajadili suala ambalo mpaka hivi karibuni lilionekana kuwa mwiko nchini Somalia - ubakaji hasa kwa wanawake wanaoishi kwenye makambi ya watu wasiokua na makazi .
    Mfanyakazi wa Kisomali wa shirika la msaada, Ali Adan ameiambia BBC kuwa, uamuzi wa kujadili suala hilo kwenye mkutano ni hatua kubwa .
    "Unyanyasaji kingono ni jambo ambalo lilikuwa halizungumziwi nchini Somalia," anasema.
    Jumuiya ya Kimataifa yenyewe imeona umuhimu wa kujadili suala hilo haraka iwezekanavyo kwa sababu limekithiri.
    Waziri Mkuu wa Uingereza na David Cameron akiwa na Rais Hassan Sheikh

    Akina mama waunga mikutano ya kutafuta amani ya Somalia, mjini London
    Wajumbe kutoka zaidi ya nchi 50 na mashirika mbalimbali wanatarajiwa kuhudhuria mkutano huo.
    Jumatatu nchi ya Qatar ilisema shambulio la bomu la Jumapili mjini Mogadishu liliwalenga maafisa wake, limearifu Shirika Rasmi la Habari la Qatar, QNA.
    Maafisa hao wanne walikuwa wakisafiri kwa kutumia gari la kijeshi la serikali ya Somali wakati msafara wao uliposhambuliwa. Hakuna raia wa Qatar aliyejeruhiwa.
    Hata hivyo, watu wengine 10 walijeruhiwa katika shambulio hilo, kwa mujibu wa mwandishi wa BBC mjini Mogadishu.

    No comments:

    Post a Comment