Ilidaiwa kuwa dereva wa gari hilo aliyejulikana kwa jina la Baraka Moleli, alikuwa akiliendesha kwa mwendo wa kasi na alikuwa akijaribu kuipita pikipiki huku abiria wake wakimshangilia.
Majeruhi na maiti walipelekwa katika Hospitali ya Mbarali ambapo Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro alifika hospitalini hapo na kusema kuwa katika ajali hiyo wanaume wanne na mwanamke mmoja walifariki dunia na kati yao watatu wametambuliwa kuwa ni Samweli Mapugilo Mbena, 30, mkazi wa Ilembula, Bon Mfupa, 27, mkazi wa Mapogolo na Edger Mwakipesile, 35, mkazi wa Nonde Mbeya.
No comments:
Post a Comment