7 Februari, 2013 - Saa 12:24 GMT

Rais wa Iran Ahmedinejad amekuwa katika majibizano na Marekani kuhusu mpango wake wa nuklia
Kiongozi wa kiroho
nchini Iran,Ayatollah Ali Khamenei, amekataa kata kata pendekezo la
Marekani kwua nchi hizo mbili zifanye mazungumzo ya ana kwa ana kuhusu
mpango wake wa nuklia.
Katika taarifa iliyocahpishwa kwenye mtandao
wake, ,Ayatollah Ali Khamenei, alinukuliwa akisema kuwa kutano kama huo
hautasuluhisha matatizo yoyote.Hili ndio jibu la kwanza la Khamenei kwa wazo la Marekani kufanya mazungumzo na Iran kuhusu mpango wake wa Nuklia.
Wazo hili lilipendekezwa na makamu wa rais wa Marekani Joe Biden wiki jana.
Hata hivyo wazo hilo lilipongezwa na waziri wa mashauri ya kigeni wa Iran.
Lakini mwenye usemi wa mwisho kuhusu mambo ya kigeni ni kiongozi huyo wa kiroho.
No comments:
Post a Comment