Muuwaji wa Padri Mushi Zanzibar akamatwa.
Jeshi
la Polisi Zanzibar limefanikiwa kumtia mbaroni kijana mmoja
anaejulikana kwa jina la Omar Mussa Makame mkaazi wa Mwanakwerekwe
mwenye umri wa miaka 35 kwa tuhuma za mauwaji ya Padri Mushi alieuwawa
kwa risasi siku ya tarehe 17\2\2013 maeneo ya Betras Zanzibar wakati
akiwa kwenye harakati za kuhudhuria ibada.
Kwa mujibu wa
taarifa kutoka kwa Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Bwana Mussa
Ali Mussa amesema kuwa kukamatwa kwa mtu huyo kumekuja baada ya Jeshi
hilo kwa kushirikiana na FBI kuchora mchoro wa mhusika wa tukio hilo
ambapo waliweza kuchora mchoro huo baada ya kupata maelezo tosha kutoka
kwa watu walioshuhudia kuwawa kwa Padri Mushi na ndio wao wakachoro
mchoro halisi wa mauwaji hayo.
Aidha Kamishna Mussa amesema kuwa hatuwa ya kufanikiwa kumkamata kijana
huyo imekuja baada ya wao kutoa mchoro sehem mbali mbali zikiwemo
mitandao mbali mbali ya kijamii na ndipo wakatokea wasamaria wema na
kusema kuwa kwa mujibu wa picha iliotolewa basi wao wanamjua mtu huyo na
ndipo walipotoa taarifa ambazo zilifanikisha Jeshi hilo kumtia mbaroni
kijana huyo.
Hata hivo Kamishna amesema kuwa hawakuridhika tu
kutokana na ushahidi huo badala yake wao kama jeshi la Polisi walifanya
gwaride maaalumu la utambuzi kwa kuwakushanya watu walioshuhudia tukio
zima na kusema kuwa ni kweli aliekamatwa ndie mhusika mkuu wa mauwaji ya
Padri Mushi.
Pamoja na hayo kamishna amefahamisha kuwa kwa
sasa wanasubiri file la mtuhumiwa huyo litoke kwa mkurugenzi wa mashtaka
ili waweze kumfikisha mtuhumiwa huyo katika vyombo husika.
Sambamba na hayo kamishna Mussa ametowa wito kwa jamii kwa ujumla kutoa
ushirikiano wa hali ya juu ili kuondoa uhalifu Nchini kwetu.
No comments:
Post a Comment