
Ndege hizo aina ya F-22 zinadaiwa kupelekwa kwenye ngome ya kikosi
cha anga huko Osan, ngome kuu ya kikosi cha anga cha Marekani nchini
Korea Kusini.
Hata hivyo, Marekani haijasema ilipeleka ndege ngapi za kivita Korea Kusini kutoka kwenye ngome yake ya kikosi cha anga cha Okinawa, Japan.
Hata hivyo, Marekani haijasema ilipeleka ndege ngapi za kivita Korea Kusini kutoka kwenye ngome yake ya kikosi cha anga cha Okinawa, Japan.
Wasiwasi uliongezeka tangu kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-Un
kuamuru jaribio la silaha za nyuklia mwezi Februari, mwaka huu.
Wiki iliyopita Korea Kaskazini ilisema kuwa inaingia katika vita na
Korea Kusini, katika mwendelezo wa vita vya maneno dhidi ya utawala
mjini Seoul na Washington.
Hii ni baada ya kuwekewa vikwazo vya kimataifa kufuatia jaribio lake
la silaha za nyuklia.Shirika la Habari la Korea Kaskazini KCNA, lilitoa
taarifa inayosema kuwa kuanzia sasa, uhusiano wa Kaskazini na Kusini
utaingia katika hali ya vita, na kwamba masuala yote yanayojitokeza kati
ya pande hizo yatashughulikiwa ipasavyo.
Tangu mwanzoni mwa mwezi huu Korea Kaskazini ilikuwa ikitishia kila
siku kuishambulia Korea Kusini pamoja na kambi za kijeshi za Marekani.
Vitisho hivi vinakuja baada ya Marekani na Korea Kusini kuanzisha
mazoezi ya kawaida ya kijeshi, na imeyaamrisha majeshi yake kukaa kwa
tahadhari na kuwa tayari kushambulia wakati wowote.
Korea Kaskazini ilitoa tishio jipya kuishambulia Marekani, baada ya ndege mbili za Marekani chapa B-2 zenye uwezo wa kubeba makombora ya nyuklia kufanya mazoezi nchini Korea ya Kusini.
Tishio la Korea Kaskazini la kuingia vitani na Korea Kusini kumezusha wasiwasi mkubwa katika rasi ya Korea.
Korea Kaskazini ilitoa tishio jipya kuishambulia Marekani, baada ya ndege mbili za Marekani chapa B-2 zenye uwezo wa kubeba makombora ya nyuklia kufanya mazoezi nchini Korea ya Kusini.
Tishio la Korea Kaskazini la kuingia vitani na Korea Kusini kumezusha wasiwasi mkubwa katika rasi ya Korea.
Wiki iliyopita Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un aliamuru
jeshi lake kujitayarisha kufuatia hatua ya Marekani na Korea Kusini
kukataa kufuta mazoezi ya kijeshi ya kiwango kikubwa yaliyopangwa
kufanywa kwa pamoja na nchi hizo mbili.
Kiongozi huyo alionya kuwa nchi yake iko tayari kukabiliana na nchi
hizo mbili baada ya ndege hizo mbili za kijeshi za Marekani kupeleka
kundi la majeshi nchini Korea Kusini.
Pyongyang inahofiwa kuwa hatua ya nchi hizo mbili – Marekani na Korea Kusini inanuia kufanya uvamizi wa kijeshi ndani ya nchi yake.
Pyongyang inahofiwa kuwa hatua ya nchi hizo mbili – Marekani na Korea Kusini inanuia kufanya uvamizi wa kijeshi ndani ya nchi yake.
Hata hivyo tayari wachambuzi nchini humo walisema ghasia kamili zikiibuka itakuwa ni njia moja ya Pyongyang kujimaliza yenyewe.
Wachambuzi hao pia walisema vitisho hivi vinanuia kuishawishi
Marekani kuingia katika meza ya mazungumzo, kumhimiza Rais mpya wa Seoul
kubadilisha sera yake dhidi ya Korea Kaskazini na kujenga umoja ndani
ya nchi bila ya kutishia vita vikubwa kati ya Kusini na Kaskazini.
No comments:
Post a Comment