Tuesday, January 15, 2013

Wizara ya Mambo ya Nje ya Somalia kuainisha, kufanya hifadhi za nyaraka kuwa za kisasa

Wizara ya Mambo ya Nje ya Somalia imetangaza mpango wa kuratibu na kufanya hifadhi yake ya nyaraka kuwa ya kisasa, ambayo iliepuka majaribio kadhaa ya kutaka kuporwa na kuharibiwa kwa kipindi cha miongo miwili iliyopita.
  • Askari polisi Abdi Mohamed Samatar akihutubia ujumbe wa maofisa wa wizara unaoongozwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Jamal Mohamed Barrow, akionyeshwa hapa akitathmini picha kutoka katika hifadhi za nyaraka. [Adnan Hussein/Sabahi] Askari polisi Abdi Mohamed Samatar akihutubia ujumbe wa maofisa wa wizara unaoongozwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Jamal Mohamed Barrow, akionyeshwa hapa akitathmini picha kutoka katika hifadhi za nyaraka. [Adnan Hussein/Sabahi]
  • Wizara ya Mambo ya Nje inapanga kuainisha na kuingiza rundo la hifadhi ya nyaraka za karatasi kuwa ya dijitali ambazo hapo kabla zilihifadhiwa ovyo kwa kipindi cha zaidi ya miaka 30 iliyopita. [Adnan Hussein/Sabahi] Wizara ya Mambo ya Nje inapanga kuainisha na kuingiza rundo la hifadhi ya nyaraka za karatasi kuwa ya dijitali ambazo hapo kabla zilihifadhiwa ovyo kwa kipindi cha zaidi ya miaka 30 iliyopita. [Adnan Hussein/Sabahi]
Sheikh Ahmed Nur, mkurugenzi wa idara ya utawala na fedha ya wizara, alisema wizara hiyo inapanga kutathmini ukamilifu wa nyaraka zake za siri, ikiwa ni pamoja na mikataba na mapatano ambayo yanahusiana na kiwanda, jeshi, ushirikiano wa sayansi na teknolojia.
"Wizara ya Mambo ya Nje ya Somalia na Ushirikiano wa Kimataifa unaangalia namna ya kuhuisha uhusiano wa kidiplomasia na jumuiya za kimataifa katika namna ambayo inatofautiana na serikali za mpito zilizopita ambazo ziliitawala nchi kwa mafanikio baada ya kuanguka kwa serikali kuu ya kijeshi iliyotawala kwa miaka 22 iliyopita," Nur aliiambia Sabahi.
"Hifadhi zetu ya nyaraka za taifa zitaweza kutupa taarifa na mwongozo kuhusu mapatano yaliyopita na deni lililobakia la Somalia, na pia akaunti za benki za nje za Somalia na mali, ambazo zinajumuisha maeneo ya biashara na majengo ya balozi na balozi ndogo," alisema. "Hii itatoa taarifa muhimu kwa wafanya uamuzi katika wizara pamoja na watafiti na wataalamu wa nyanja mbalimbali, hususani uhusiano wa kimataifa."
Nur alisema asasi ya hifadhi za nyaraka itashirikiana na uundaji mpya mkubwa wa wizara, ikiwa ni pamoja na mradi wa kisasa ili kuziwekea ofisi zake kompyuta, upatikanaji wa intaneti, kamera za uchunguzi, skana za utambuzi kwa wafanyakazi wa wizara, vifaa vya elimu ya lugha na masomo ya kidiplomasia, na majenereta ya umeme.
Mwanadiplomasia mstaafu Abubakar Adow, mshauri wa Wizara ya Mambo ya Nje, alisema mradi huo mpya utasaidia wizara wakati inajitayarisha kubadilisha upya muundo wa wafanyakazi wake nchini Somalia na ujumbe wa kidiplomasia nchi za nje.
"Tuna fursa ya kweli," aliiambia Sabahi. "[Kwa msaada wa fedha kutoka] serikali rafiki na mashirika ya maendeleo, waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa kimataifa anaweza kuwa na hifadhi pana ya nyaraka inayozingatia viwango vya sasa vya kimataifa na vigezo, hivyo kuhakikisha utunzaji wa nyaraka ili zisiharibike au kupotea."
Adow alisema wizara inataka kuunda idara ya hifadhi kuu ya nyaraka ili kuandaa na kuweka katika dijiti makala za kihistoria na kuajiri na kuwafundisha wafanyakazi kusimamia kumbukumbu.
Polisi Abdi Mohamed Samatar, ambaye ni kiongozi wa kitengo ambacho kinalinda wizara, alisema yeye na wanajeshi wengine wawili wamefanya kazi tangu miaka ya 1980 kulinda hifadhi ya nyaraka.
"Wanamgambo hutufyatulia risasi wakitumia bunduki zao za rashasha," aliiambia Sabahi. "Wakati wa tukio hilo mwezi Aprili 1995, nilipigwa risasi na ilibidi nikae katika Hospitali ya Medina, ambayo iko karibu na wizara, kwa siku 25 kabla ya kuodoka."
Kitengo kidogo cha Samatar pia kilipambana mara kadhaa na wanamgambo wa kikabila kutaka kuchukua majengo ya wizara na kuyageuza nyumba za kuishi au maduka ya biashara. "Tumekuwa makini sana kuhusu shughuli hizo ambazo si kwa maslahi ya umma," alisema.
Samatar alisema Muungano wa Mahakama za Kiislamu (ICU) ulichukua jengo la Wizara ya Mambo ya Nje mwaka 2006 na kuondoa hifadhi za nyaraka na kuyagawa majengo ya wizara. Wanaharakati walizuia misheni hiyo, hata hivyo, kwa kuishawishi ICU kwamba hifadhi ya nyaraka inatoa kumbukumbu za kihistoria kwa vizazi vijavyo.

No comments:

Post a Comment