Tuesday, February 5, 2013

AFISA MDHAMINI WIZARA YA MIUNDO MBINU NA MAWASILIANO AJERUHIWA KWA MAPANGA KISIWANI PEMBA

 
 
 
 
 
 
Rate This

Imewekwa na Mhamed Khamis
Mandhari ya Mji  wa Wete kisiwani Pemba
Mandhari ya Mji wa Wete kisiwani Pemba
Licha ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kukemea mara kadhaa pamoja kutoa adhabu kwa wale wamnaopatikana na hatia kuwa wamehusika na matendo maovu ikiwemo ujambazi lakini hali bado inazidi kuwa mbaya kutokana na kukisiri kwa matendo hayo.

Hayo yamekuja kufuatia Afisa Mdhamini na Mawasiliano kisiwana Pemba Bwana Hamadi Ahmed Baucha  kuvamiwa usiku wa kuamkia jana na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi huko nyumbani kwake kifumbika Wete Pemba.

Afisa huyo amesema kuwa watu hao waliokuwa na Mapanga walivamia na kumjeruhi zsehemu kadhaaa ndani ya mwili wake ikiwemo kwenye mgongo lakini kw hawakufanikiwa kupata lolote ndani ya Nyumba hio.
Aidha amesema licha ya kupata majeraha kadhaa lakini hali yake ka sasa inaendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu katika hospitali ya Wete.

Kwa upande wake kamabda a Polisi kaskazini Pemba Bwana Yahya Rashid Bugi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na ameiomba jamii kutoa ushirikiano ipasavo pale wanapowaona watu wasiowajua ndani ya jamii zao ili hatuwa za uchunguzi zichukuliwe juu yao kwani hwenda ikawa ndio miongini mwa wanaofanya matendo mabaya

No comments:

Post a Comment