Monday, February 18, 2013

CUF YALAANI VIKALI TUKIO LA KUWAWA KWA PADRI ZANZIBAR

 
 
 
 
 
 
Rate This

Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF,Professa Ibraim Lipumba
.
Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF,Professa Ibraim Lipumba
Kufuatia tukio la kuuwawa kwa Padri Muche kwa kupiigwa Risasi huko Mtoni Zanzibar wakati akiwa kwenye harakati za kuhudhuria katika ibada ya misa Chama cha Wananchi CUF kimelaani vikali kitendo hicho n cha kiyama  kwani ni kinyume na ubinadamu
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Habari uenezi na mawasiliano ya Umma MH: Salim Biman kwa niaba ya Mwenyekiti wa Chama hicho Pr ,Ibrahim haruna Lipumba   kutokana na kuchukizwa vikali na tukiuo la kinyama lililofanywa na baadhi ya watu wachache wenye nia mbaya na Nchi ya Zanzibar.
Kutokana na tukio hilo Chama cha wananchi Cuf kupitia Mkurugenzi wa habari wa chama hicho imemelitaka Jeshi la Polisi Nchini kuwa makini na matukio ya kiuhalifu yanayotokea siku hadi siku ambayo yanatowa taaswira mbaya kwa wananchi wenyewe na wageni wanaokuja kutoka nje.
Pia amelitaka jeshi hilo kwa kushirikiana na Usalama wa Taifa kuendesha uchunguzi wa kina na waharaka  ili kuhakikisha litawatia mbaroni wahusika wote wa tukio hili ili kuinusuru Nchi kuingia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Hivyo  ametoa pole kwa waumini wa dini ya kikirsto na kuwataka wawe na moyo wa subra katika kipindi hichi kigumu kwao nawawe watulivu  suala hili waiachie mamlaka husika kulipatia ufumbuzi  wa tatizo hili.
Mh Bimani pia amewataka wanachi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Jeshi la Polisi ili kuhakikisha linawafichuwa wahalifu wote badal ya kuhifadhiwa kwani ni wahujumu wa taifa.
Chama cha wananchi  kinaimani kuwa,wananchi waliowengi wamepatwa na huzuni pamoja na mshituko mkubwa mkubwa kufuatia tukio hilo,hivyo hali hiyo inwakosesha raha na imani ya kuishi kama ilivyo zamani.

No comments:

Post a Comment