Watu waliokuwa na silaha katika
jimbo la Bauchi, kaskazini mwa Nigeria, wamewateka nyara mafundi wa
ujenzi saba kutoka nchi za nje.

Wafanyakazi kutoka Utaliana, Ufilipino, Uingereza, Uguriki na Libnan inasemekana ni kati ya wale waliotekwa nyara.
Kabla ya hapo kituo cha polisi katika mji wa Jama'are kiliingiliwa.
Polisi wa Nigeria hawakuweza kutambua waliofanya shambulio hilo lakini waandishi wa habari wanasema wanaoshukiwa ni kundi la wapiganaji wa Kiislamu, Boko Haram.
No comments:
Post a Comment