Thursday, February 21, 2013

JIHADI ”UVUVI HARAMU NI MOJA KATI YA VITENDO VINAVOKWAMISHA JUHUDI ZA SERIKALI”

 
 
 
 
 
 
Rate This

Imewekwa na Mhamed khamis
WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI ABDILAHI JIHAD HASSAN AKIWA AMEBEBA KASA AKIELEKEA BAHARINI KUMACHIA HURU.
WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI ABDILAHI JIHAD HASSAN AKIWA AMEBEBA KASA AKIELEKEA BAHARINI KUMACHIA HURU.
        Waziri wa Mifugo na  Uvuvi Mh. Abdilahi Jihad Hassan amesema uvuvi haramu ni miongoni mwa vitendo vinavyokwamisha jitihada za serikali katika utunzaji wa mazingira na viumbe  wa asili wa baharini.

Hayo ameyasema wakati akizungumza katika sherehe za kuwaachia huru kasa huko katika hifadhi ndogo ya viumbe hao nungwi.

          Amesema  ili kudhibiti hali hiyo lazima  wananchi  hasa wavuvi waachane na tabia ya kutumia mbinu duni ya uvuvi haramu inayochangia kuaharibu mazingira na kupoteza uhai wa viumbe wanaoishi baharini .

       Mh.jihad amesema wakati umefika kwa jamii kuheshimu sheria zilizopo zikiwemo za uvuvi na uhifadhi wa mazingira ili matumizi ya rasilimali za bahari ziwe endelevu kwa maslahi ya wananchi na vizazi vijavyo.
        Ametoa wito kwa jamii kuacha kutumia kasa kama kitoweo kwani kufanya hivyo ni kupoteza jamii ya viumbe hao muhimu katika ukanda wa bahari ya visiwa vya zanzibar.
         Katika Risala ya Jumuiya ya Uhifadhi wa Kasa ya Nungwi  “Mnarani Natural Aquarium” imesema inakabiliwa na matatizo mbalimbali ikiwemo ukosefu wa elimu ya kisasa juu ya ufugaji wa viumbe hao,bwawa la kufugia kasa kujaa tope mara kwa mara pamoja na upungufu wa fedha za kuendeshea miradi ya jumuiya hiyo.
        Jumuiya hiyo inafuga viumbe wa baharini na nchi kavu wakiwemo kasa ,kaa,chatu na mijusi aina ya kenge pamoja na mabaki ya samaki mkubwa duniani aina ya nyangumi pia katika hafla hiyo jumla ya kasa 20 wameachiwa huru katika maeneo ya bahari.

No comments:

Post a Comment