Jumuiya
ya Mabohora mkoa wa Morogoro imeadhimisha miaka 102 ya kuzaliwa
Kiongozi wao mkuu wa Jumuiya hiyo Duniani Syedna Mohammed Burhanuddin
kwa kupanda miti mia moja ya aina mbalimbali ikiwemo ya matunda kwa
lengo la kuhifadhi mazingira.
Sheikh
Mkuu wa Mabohora Mkoa wa Morogoro, Zoeb Bhai,anasema katika kuadhimisha
siku ya kuzaliwa ya kiongozi wao mkuu, wameamua kupanda miti katika
maeneo ya viwanja vya manispaa, Shule ya Msingi Bungo na nje ya msikiti
wao
Sheikh
wa Jumiya ya Mabohora wa Mkoa wa Morogoro, Zoeb Bhai na wanajumuiya
hiyo wanaeleza kuwa kutokana na upendo na kumuenzi kiongozi wao huyo
wataendelea kupanda miti mingine mia moja ya aina hiyo katika kijiji cha
Mkundi kilichopo katika manispaa hiyo ambacho kimeanza kuathirika
kimazingira.
Naye
mkurugenzi wa manispaaya Morogoro Jervis Simbeye ameipongeza Jumuiya
hiyo ya Mabohora kwa kuadhimisha siku ya kuzaliwa ya kiongozi wao mkuu
Duniani kwa kupanda miti.
Monica Lyampawe, TBC Morogoro
No comments:
Post a Comment