Mahakama moja ya Misri yamepiga
marufuku kwa mwezi mmoja tovuti ya kusambaza video ya Youtube kwa
kuonesha filamu iliyotusi Uislamu na kuzusha maandamano ya ghasia katika
sehemu kadha za nchi za Kiislamu.

Kesi hiyo ilipelekwa mahakamani na wakili mmoja wa Misri, Hamed Salem, ambaye amewahi kushtaki mashirika mengine ya habari na watu wanaoonekana kuwa wanatusi Uislamu.
Mwezi uliopita mahakama moja ya Misri ilithibitisha hukumu ya kifo kwa Wamisri wasiokuwako mahakamani, kwa kuhusika na filamu hiyo.
No comments:
Post a Comment