
Hayo yalisemwa jijini Dar es Salaam jana na Waziri wa Katiba na
Sheria, Mathias Chikawe, alipokuwa akifungua mkutano wa Kamati Tendaji
za Tume za uchaguzi za nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika
(SADC) wenye lengo la kubadilishana mawazo na kujifunza mambo mbalimbali
yanayohusu mifumo ya uchaguzi.
“NEC na ZEC mnatakiwa kujipanga kikamilifu kusimamia zoezi hilo na kupokea mabadiliko kwa mtazamo chanya,” alisema Chikawe.
Katika mchakato wa katiba mpya Tume ya Mabadiliko ya Katiba baada
ya kukusanya maoni yaliyotolewa na wananchi kwa sasa inayachambua ili
kuandaa rasimu ya Katiba ifikapo Juni mwaka huu.
Baada ya rasimu hiyo kuandaliwa itapelekwa katika Bunge Maalum la
Katiba na Watanzania wote watapiga kura ya maoni kupitisha katiba hiyo
ama kuikataa.
Alisema ingawa ni muhimu kujenga demokrasia, lakini chaguzi za
Afrika zimekuwa zikifanyika na wakati mwingine kutokea ugomvi, migogoro
na vita inayosababishwa na uwezo mdogo wa kusimamia michakato ya
chaguzi.
CHANZO: NIPASHE
No comments:
Post a Comment