Thursday, February 28, 2013

Zaidi ya bilioni 5 kutumika kutengeneza barabara Z,bar

 
 
 
 
 
 
Rate This

njia
Ni ukweli usiofichika kuwa moja miongoni mwa nyenzo muhimu za maendeleo ni kuwepo kwa mawasiliano ya barabara kwani huweza kuwarahisishia jamii husika kupata mawasiliano kwa muda mfupi.
Zaidi ya shillingi bilioni tano zimetengwa kutumika kwa ajili ya matengenezo ya barabara za Unguja na Pemba katika kipindi cha mwaka huu.
 Mkurugenzi wa idara ya ujenzi na utunzaji barabara zanzibar Bw Ali Twahir Fatawi amesema kuwa fadha hizo zitatumika kukamilisha ujenzi wa barabara ya amani mtoni yenye urefu wa kilomita nne na barabara ishirini za ndani Unguja na Pemba 
Ameyasema hayo wakati akizungumza na mwandishi wetu  katika ujenzi huo utaweza kuhusisha utiaji wa lami, kifusi pamoja na matengenezo mengine kwenye barabara mbali mbali zilizopo Zanzibar.  
 Bw fatawi akizungumzia kuhusu suala la  utunzaji wa barabara inashirikiana na vikundi vya kijamii kuweka mipango ya uhifadhi wa barabara ili zidumu kwa muda mrefu.

No comments:

Post a Comment