Thursday, February 28, 2013

Ukuwaji wa watoto upo hatarini iwapo hawatokingwa-Juma Duni

 
 
 
 
 
 
Rate This

duniWaziri wa afya  Mhe Juma Duni amesema ukuaji wa watoto uko hatarini iwapo hakutakuwa na juhudi za kuwakinga na  maradhi mbalimbali yanayohatarisha maisha yao.
Amesema kutokana na hali hiyo kunahaja ya kuwalinda watoto hao ambao ni tegemeo la maendeleo ya taifa la baadae.
Akizindua huduma ya chanjo  ya  ugonjwa wa  kuhariha, nemonia  na uti wa mgongo inayotolewa kwa watoto chini ya mika mitano mhe duni amesema huduma hiyo iliyoanza kutolewa kwa wiki tatu sasa  itasaidia     kupunguza maradhi hayo ambayo ni hatari kwa watoto.
Mh juma duni amewasisitiza wazazi kushirikiana na watendaji wa sekta ya afya ili kuhakikisha watoto wao wanapatiwa chanjo kwa wakati.
 Nae  mratibu wa chanjo za Mama na watoto zanzibar bw Yussuf Haji Makame amesema jamii imekuwa na uelewa mkubwa juu ya kinga mbalimbali zinazotolewa kwa watoto na wamejiepusha  katika imani za potofu.
 Amesema chanjo hizo  za  ugonjwa wa  kuhariha, nemonia  na uti wa mgongo zitatolewa kwa awamu mbili   kwa watoto wenye umri kuanzia wiki sita  hadi   wiki kumi.

No comments:

Post a Comment