Tuesday, March 26, 2013

Maporomoko yasababisha vifo Indonesia

 25 Machi, 2013 - Saa 09:23 GMT
Waokoaji nchini Indonesia
Waokoaji nchini Indonesia
Watu sita wamefariki na wengine 18 hawajulikani walipo baada ya ardhi kuporomoka katika kisiwa cha Java nchini Indonesia.
Mamia ya polisi, wanajeshi na umma wamekuwa wakichimba magofu wakiwatafuta manusuru.
Kama ilivyo desturi nchini Indonesia, mvua kubwa ya msimu husababisha maporomoko ya ardhi kila mwaka.
Brazil
Na huko Brazil pia, mvua kubwa imesababisha mafuriko na kuvuruga maisha ya wakaazi wa jimbo la Rio de Janeiro.
Katika mji wa Angra dos Reis, watu 3,000 walikatiwa mawasiliano wakati daraja muhimu linalowaunganisha na miji mingine lilipokatika.
Miporomoko miwili ya ardhi pia iliwazuia watu kufika mjini humo.
Maporomoko ya ardhi yamewauwa makumi ya watu katika majuma kadhaa yaliyopita eneoni humo.

No comments:

Post a Comment