25 Machi, 2013 - Saa 07:02 GMT

Wateja wapiga foleni ili kutoa pesa
Mawaziri wa fedha wa Eurozone
wamekubali kuipa Cyprus mkopo wa euro bilioni 10 ili kuzuia mfumo wake
wa benki usiangamie, na pia kuhakikisha kwamba nchi hiyo inabaki katika
eneo la eurozone.
Benki ya Laiki – benki ya pili kwa ukubwa nchini
– itafungwa taratibu. Wateja watakaoathirika zaidi ni wale waliohifadhi
zaidi ya euro 100,000, amabo yasemekama watakatwa fedha fulani.Kamishna wa Masuala ya Kiuchumi ya EU, Olli Rehn, amesema kwamba "kina cha matatizo ya kifedha nchini Cyprus chamaansisha kwamba hali ya baadaye itakuwa ya shida kwa nchi hiyo na watu wake".
Nalo Benki la Cyprus – benki kubwa kabisa kisiwani humo – Jumapili iliwakubalia wateja watoe kiasi cha euro 120 kwa siku tu toka mashine za kutolea pesa za ATM.
Foleni ndefu zilionekana za watu wakitoa pesa. Benki zimefungwa tangu Jumatatu iliyopita.
No comments:
Post a Comment