Monday, March 4, 2013

Waasi 20 wa Boko Haram wauawa Nigeria

 4 Machi, 2013 - Saa 11:52 GMT
Maafisa wa polisi
Jeshi nchini Nigeria linasema kuwa limewauwa wapiganaji 20 wa kundi la Kiislam la Boko Haram katika jimbo la kaskazini magharibi mwa nchi hiyo la Borno.
Msemaji wa jeshi amesema kuwa wapiganaji hao waliuawa walipokuwa wakijaribu kushambulia kituo cha kijeshi.
Walidhibitiwa vilivyo na wanajeshi. Silaha na risasi pia zilipatikana. Lakini msemaji wa jeshi hakusema lolote kuhusu maafa.
Kundi la Boko Haram limelaumiwa kwa kufanya mashambulizi kadhaa makali huko kaskazini mwa Nigeria kwa miaka kadhaa sasa.

No comments:

Post a Comment