Monday, January 14, 2013

Masauni Wanaotetea muundo wa Muungano mkataba na Serikali mbili wanataka kuvunja Muungano

MASAUNI



 
 
 
 
 
 
Rate This

 
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimesema kitaendelea kuimarisha mahusiano yake na taasisi mbalimbali za kijamii na zile za kimataifa ili kuendeleza mashirikiano yaliyopo kwa lengo la kukiimarisha chama hicho.
Akizungumza na vijana wa CCM walio vyuo vikuu mbalimbali nchini Katibu wa Idara ya siasa, Itikadi na Uhusiano wa Kimataifa Nd, Hamad Yussuf Masauni huko Afisi kuu ya CCM Kisiwandui amesema, kuimarisha mashirikiano na taasisi hizo kutakijengea msingi imara chama hicho katika kuongoza dola.
Nd, Masauni amesema kuwa Idara ya siasa, Itikadi na Uenezi haina budi kufanya kazi kwa bidii ili kukifanya chama hicho kupata ushindi katika uchaguzi mkuu ujao.
Aidha Nd, Masauni amewataka vijana hao kuendelea kutetea sera ya chama chao katika mfumo wa muundo wa Muungano kuwa wa serikali mbili kwani ndio wenye maslahi kwa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.
Pia amesema kuwa wanaotetea mfumo wa Muungano wa mkataba na Serikali tatu wana lengo la kuvunja Muungano jambo ambalo ni hatari kwa usalama wan chi na wananchi wake hivyo hapana budi kupingwa kwa nguvu zote ili kuepusha athari zinazoweza kutokea.
Akizungumzia faida za Muungano Nd, Masauni amesema kuwa Muungano uliopo unfaida kubwa ikiwamo kukuwa kwa uchumi wa nchi pamoja na kuimarika kwa mahusiano ya muda mrefu baina ya Zanzibar na Tanzania Bara hivyo amewataka vijana hao kuendelea kuutetea ili kuzidi kuimarisha Uchumi wa Nchi.
Pia amewataka vijana hao kutumia kutumia taakuma waliyo nayo kuandaa makongamano na midahalo mbalimbali ili kutoa taaluma kwa Wananchi juu ya faida zinazopatikana ndani ya Muungano kwani wao ndio nguvu kazi ya Chama na tegemeo kwa Taifa.

No comments:

Post a Comment