Watu wenye silaha walimpiga risasi na kumuua afisa mmoja wa polisi wa
Kenya mjini Garissa usiku wa Jumatatu (tarehe 4 Februari), maafisa wa
polisi waliiambia Sabahi.
Wauaji hao wanashukiwa kuwa na mafungamano na al-Shabaab, na wanaweza
kuwa sehemu ya genge linalowalenga maafisa wa usalama wa Kenya kwenye
eneo hilo, alisema mkuu wa wilaya ya Garissa Mohamed Maalim.
Maalim alimtaja afisa huyo kuwa ni Sajenti Mohammed Bolu Wako wa
kitengo cha upelelezi cha Polisi wa Utawala katika kambi za wakimbizi za
Dadaab.
"Alikuwa ndio kwanza amewasili kutoka Nairobi kuripoti kwenye kituo
chake cha kazi siku ya Jumatano," Maalim aliiambia Sabahi. "Alikuwa
anafanya kazi zake nje ya hoteli karibu na kituo cha mabasi alipopigwa
risasi."
Maalim alisema polisi wamekuwa wakiwahoji mashahidi ili kujua lengo
la mauaji hayo. Aliwatolea wito wakaazi wa huko kuwasaidia polisi
kuwatambua na kuwakamata wauaji.
Al-Shabaab imewakodi wenyeji wa huko kuwalenga wanajeshi na polisi wa Kenya,
alisema Maalim kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation la Kenya.
"Haiwezekani kwa al-Shabaab kutoka Kismayu na kuja kuanza kuua watu
hapa," alisema. "Wahalifu hawa wanakodiwa na kundi hilo la kigaidi
kusababisha mvutano katika mji huo."
No comments:
Post a Comment